Simeoni wa Mnarani Kijana

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Simeon Stylites the Younger)
Picha takatifu ya Kiorthodoksi ya Mt. Simeoni.

Simeoni wa Mnarani Kijana (kwa Kiarabu مار سمعان العمودي الأصغر mār semʻān l-ʻamūdī l-asghar; Antiokia, leo nchini Uturuki, 521 - Antiokia, 24 Mei 592) alikuwa mkaapweke aliyepata umaarufu kwa kuishi miaka 68 juu ya minara mbalimbali akianzia utotoni[1] kwa kufuata mfano wa Yohane, kiongozi wake wa kiroho.

Alipohama mnara mmoja kwenda mwingine alipata nafasi ya kupewa ushemasi halafu upadri.

Mbali na kutenda miujiza mingi, aliacha maandishi mbalimbali[2].

Umeongezewa sifa "kijana" ili kumtofautisha na waliofuata mtindo wake huo kama Simeoni wa Mnarani Mzee, Simeoni wa Mnarani III na Simeoni wa Mnarani wa Lesbos[3].

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, Wakatoliki na Waanglikana kama mtakatifu kama mama yake, Marta wa Antiokia.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 24 Mei [4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. It is Simeon himself who in his letter to Thomas states that he was living upon a pillar when he lost his first teeth.
  2. Besides the letter mentioned, several writings are attributed to the younger Simeon. A number of these small spiritual tractates were printed by Cozza-Luzi ("Nova PP. Bib.", VIII, iii, Rome, 1871, pp. 4–156). There is also an "Apocalypse" and letters to the Emperors Justinian I and Justin II (see fragments in P.G., LXXXVI, pt. II, 3216-20). More especially Simeon was the reputed author of a certain number of liturgical hymns, "Troparis", etc. (see Pétridès in "Échos d'Orient", 1901 and 1902).
  3. https://www.santiebeati.it/dettaglio/92678
  4. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.