Siku ya Kimataifa ya Lughamama

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Shaheed Minar, au kumbukumbu la mashahidi, kwenye Chuo Kikuu cha Dhaka, Bangladesh, inayofanya ukumbusho wa wanafunzi waliokufa kwa ajili ya lugha ya Bangla tarehe 21 Februari 1952

Siku ya Kimataifa ya Lughamama inayoadhimishwa tarehe 21 Februari ilitangazwa na UNESCO tarehe 17 Novemba 1999. Tangu tarehe hiyo imetambuliwa pia na Umoja wa Mataifa katika azimio lake la tarehe 16 Mei 2007, lililotangaza mwaka wa 2008 kuwa Mwaka wa Lugha wa Kimataifa.[1]

Asili ya Siku ya Lughamama ni tukio la mwaka wa 1952 nchini Bangladesh, wanafunzi wa chuo kikuu cha Dhaka walipofanya maandamano kwa ajili ya Kibengali, na wengine wao kuuawa na polisi kwa kupigwa risasi.

Siku ya Lughamama husherehekewa na nchi zilizojiunga na UNESCO kila mwaka tangu mwaka wa 2000, kwa ajili ya kujadili mambo ya wingi wa lugha, haki za lugha zote, na mazingira ya kutumia lugha tofauti.

Mada za kila mwaka[hariri | hariri chanzo]

Kwa kawaida, Siku ya Lughamama ina mada tofauti kila mwaka.[2]

  • 2000: Sherehe ya kwanza
  • 2001: Sherehe ya pili
  • 2002: Wingi wa lugha: lugha elfu tatu ziko hatarini kufa
  • 2003: Sherehe ya nne
  • 2004: Elimu ya watoto[3])
  • 2005: Lugha kwa wasioona na kwa wasionena
  • 2006: Lugha na Mtandao
  • 2007: Elimu kwa lugha nyingi
  • 2008: Mwaka wa Lugha wa Kimataifa
  • 2010: Mwaka wa Kimataifa wa Ubunifu wa Tamaduni
  • 2011: Teknolojia ya habari na mawasiliano
  • 2012: Maelekezo ya Lugha Mama na Kujumuishwa kielimu
  • 2013: Vitabu vya elimu ya lugha ya mama
  • 2014: Lugha za asili kwa uraia wa ulimwengu: uangalizi kwenye sayansi
  • 2015: Ujumuishwaji ndani na kupitia elimu (na Kongamano Jijini Parisi)[4]
  • 2016: Elimu Bora, Lugha ya kufundishia na kujifunza matokeo
  • 2017: Matarajio endelevu kupitia elimu ya lugha nyingi
  • 2018: Lugha zetu, mali zetu.
  • 2019: Mwaka wa kimataifa wa Lugha asilia[5]
  • 2020: Kulinda utofauti wa lugha

Matukio mengine[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Ona pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Siku ya Kimataifa ya Lughamama kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.