Sigujana
Mandhari
Sigujana kaSenzangakhona (alifariki 1816) alikuwa Mfalme wa Wazulu mwaka 1816. Alikuwa mwana wa Senzangakhona kaJama na nusu ndugu wa Dingane kaSenzangakhona na Shaka kaSenzangakhona. Alirithi kiti cha kifalme cha baba yake karibu na mwaka 1816.[1] Mama yake alikuwa Bhibhi kaSompisi. Mara baada ya kuwa kiongozi, aliuawa na nusundugu yake, Shaka Zulu. Haijulikani wazi kama Shaka aliwaua kwa mpango wa kikatili,[1] au Shaka mwenyewe alimchoma Sigujana kwa kisu.[2] Tarehe ya kuzaliwa kwake haijulikani, lakini alifariki mwaka 1816, muda mfupi baada ya kuwa Mfalme.
Marejeleo
[hariri | hariri chanzo]- 1 2 Lipschutz, Mark R.; Rasmussen, R. Kent (1986). "Senzangakhona". Dictionary of African Historical Biography (tol. la 2nd). University of California Press. uk. 213. ISBN 0-520-06611-1.
- ↑ Eldredge, Elizabeth A. (2014). The Creation of the Zulu Kingdom, 1815–1828. Cambridge University Press. ku. 74–75. ISBN 978-1-107-07532-0.
| Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Sigujana kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |