Siasa ya Tanzania
|
Nembo ya Taifa ya Tanzania | |
| Aina ya Serikali | Jamhuri ya urais ya vyama vingi |
| Rais wa Nchi | Samia Suluhu Hassan |
| Makamu wa Rais | Philip Mpango |
| Chama Tawala | Chama Cha Mapinduzi (CCM) |
| Vyama Vikuu | CCM, CHADEMA, ACT-Wazalendo, CUF, NCCR-Mageuzi, UDP |
| Uchaguzi wa Mwisho | 28 Oktoba 2020 (Urais, Bunge) |
| Uchaguzi Ujao | Oktoba 2025 (Urais, Bunge, Mitaa) |
| Katiba | Katiba ya mwaka 1977 (iliyorekebishwa mara kadhaa) |
| Tanzania |
Makala hii imepangwa kwa mfululizo: |
|
|
|
|
Nchi zingine · Atlasi |
Siasa ya Tanzania inategemea mihimili mitatu: Serikali, Bunge, na Mahakama.[1]
Serikali
[hariri | hariri chanzo]Serikali ya Tanzania ina jukumu la kutekeleza sheria na sera za nchi. Inaongozwa na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye anahudumu kama mkuu wa nchi na mkuu wa serikali. Waziri Mkuu na Makamu wa Raisi pia wanasaidia katika mhimili wa Serikali. Mhimili wa Serikali umegawanywa zaidi katika wizara, ambazo kila moja inawajibika kwa eneo maalum la sera ya serikali. Mawaziri hao huteuliwa na Rais na wanawajibika kwa shughuli za kila siku za wizara zao. Kila wizara pia inaongozwa na Katibu Mkuu ambaye ndiye mtendaji mkuu wa wizara hiyo.
Katiba ya Tanzania inaruhusu Rais kuteua wabunge 10. Wanaweza kuwa wajumbe wa baraza la mawaziri, pia. Mhimili wa Serikali katika nchi ya Tanzania una jukumu la kusimamia maendeleo ya uchumi wa nchi, mambo ya nje, ulinzi na usalama wa ndani. Unafanya kazi ya kutunga sera zinazolenga kukuza uchumi, kuboresha viwango vya maisha na kupunguza umaskini. Pia unafanya kazi ya kudumisha amani na utulivu ndani ya nchi, na kujenga ushirikiano imara na nchi nyingine katika kanda na kwingineko.
Bunge
[hariri | hariri chanzo]Huu ni mhimili wa kutunga sheria ambao una viti 393 katika Bunge moja la Kitaifa. Zanzibar ina Baraza lake la Wawakilishi la kutunga sheria hasa za Zanzibar. Wabunge wa Bunge la Tanzania wanachaguliwa kwa wakati mmoja kwa kura za moja kwa moja za wananchi kwa vipindi vya miaka mitano mitano. Kuna bunge moja katika Tanzania (bunge la Muungano). Kuna wabunge 295 katika Bunge la Kitaifa.
Mahakama
[hariri | hariri chanzo]Tanzania ina mahakama ya ngazi tano, ambayo inajumuisha mamlaka ya sheria za kawaida, za kikabila, Kiislamu na Kiingereza. Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama ya Juu huteuliwa na Rais. Tawi la Mahakama linajitegemea kutoka kwa watendaji na wabunge.
Watu
[hariri | hariri chanzo]Raisi wa sasa wa Tazania ni Dkt. Samia Suluhu Hassan. Yeye ni Raisi wa kwanza mwanamke nchini Tanzania. Waziri Mkuu wa sasa wa Tanzania ni Majaliwa Kassim Majaliwa. Na Makamu wa Raisi wa Tanzania anaitwa Philip Isdor Mpango. Raisi anaishi zaidi katika ikulu ya Dar es Salaam, ingawa ipo ikulu nyingine tayari katika mji mkuu mpya, Dodoma.
Uchaguzi
[hariri | hariri chanzo]Chaguzi nchini Tanzania hufanyika katika ngazi ya serikali za mitaa na kitaifa. Serikali za mitaa hufanya uchaguzi wa wenyeviti wa mitaa au vijiji. Uchaguzi mkuu humchagua Raisi, Wabunge wa Bunge na Madiwani. Rais huwa anachaguliwa kwa muhula wa miaka mitano, na kuweka kuchaguliwa tena kwa miaka mitano tu.
Chama cha Mapinduzi (CCM) ni chama cha siasa kikubwa na maarufu zaidi nchini Tanzania. Kati ya vyama vingine 18, kikubwa ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo, lakini, hakijawahi kushika dola.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Parliament of Tanzania". www.parliament.go.tz. Iliwekwa mnamo 2025-04-28.
| Makala hii kuhusu mambo ya siasa bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Siasa ya Tanzania Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |