Shewalul Mengistu
Shewalul Mengistu (kwa Kiamhari : ሸዋሉል መንግሥቱ; 11 Septemba 1944 - 26 Mei 1977) [1] alikuwa mshairi, mtunzi wa nyimbo, mwandishi wa habari na mwanaharakati wa kisiasa wa Ethiopia aliyeuawa mwaka wa 1977.
Familia
[hariri | hariri chanzo]Mengistu alizaliwa Hararghe, nchini Ethiopia, [1] katika familia ya tabaka la kati. Baba yake alikuwa mwanamuziki aliyepiga bägäna, kinubi chenye nyuzi kumi. Mengistu aliolewa akiwa na umri wa miaka 13 kwa kamanda katika vikosi vya usalama vya Ethiopia. Walizaa watoto watano na baadaye wakapeana talaka.
Kazi
[hariri | hariri chanzo]Mnamo mwaka 1973, Mengistu aliajiriwa na Wizara ya Habari huko Addis Ababa, ambapo aliandaa vipindi vya redio na televisheni vilivyokusudia kundi la wanawake wa Kiethiopia.
Mengistu alizungumza Kiamhari na Kioromo na aliandika wimbo Erè Mèla Mèla, unaojulikana zaidi ulipoimbwa na Mwimbaji Mahmoud Ahmed. [2] Pia alikua mwandishi wa siasa, kazi zake zikiwa ni pamoja na kuandika mashairi kadhaa (moja ambayo ilikuwa imepigwa marufuku kutangazwa na kuchapishwa) na kitabu kinachokosoa jamii ya Waethiopia.
Kifo
[hariri | hariri chanzo]Alikuwa mwanachama wa chama cha Marxist-Leninist cha Mengistu Haile Mariam, ambaye baadaye akawa dikteta. Aliuawa huko nchini Ethiopia Addis Ababa mnamo 1977, akafa baada ya kupigwa risasi.
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- 1 2 Clerfeuille, Sylvie (2019-12-02). "Shewalul Mengistu". Afrisson (kwa Kifaransa). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2025-04-26. Iliwekwa mnamo 4 Februari 2025.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ Mahmoud Ahmed - Ere Mela Mela (kwa Kifaransa), 1986, iliwekwa mnamo 2025-02-15