Nenda kwa yaliyomo

Sheba Tavarwisa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Sheba Tavarwisa (alizaliwa 1 Agosti 1946[1]) alikuwa shujaa wa vita kutoka Zimbabwe. Alikuwa miongoni mwa wanawake wa kwanza kuwa viongozi wa jeshi la kisiasa la Zimbabwe African National Union (ZANLA), ambalo liliongoza mapinduzi ya nchi dhidi ya utawala wa kikoloni.[2]

Mapinduzi

[hariri | hariri chanzo]

Tavarwisa aliwahi kufanya kazi kama mwalimu wa shule ya msingi hadi alipoacha kazi hiyo kujiunga na Jeshi la Ukombozi la Zimbabwe African National Liberation Army (ZANLA) ili kupigania uhuru wa nchi.[3] Alikuwa miongoni mwa wakaguzi wa mwanzo na viongozi wa kike wa kwanza wa harakati hiyo. Wajibu wake wa awali ulikuwa kubeba na kusambaza silaha kutoka Zambia kwenda Msumbiji hadi kwenye mstari wa mbele nchini Zimbabwe (zamani Rhodesia). Pia alikuwa na jukumu la kusambaza ujumbe wa harakati hiyo. Alishirikiana hasa na wakulima ili kupata msaada wao.[4] Tavarwisa pia alihakikisha kwamba wanawake waliokuwa katika kambi hawakudhuriwa kingono au kutumika vibaya.

Tavarwisa aliwafunza wanachama, alitekeleza misheni na kuongoza mapinduzi kama kiongozi huku akipanga muda wa kushughulikia watoto wake.

Mwaka 1978, Tavarwisa aliteuliwa kuwa Naibu Katibu wa Elimu wa ZANU. Aliendelea kupanda ngazi za uongozi na kuwa mwanachama wa tume ya juu ya uamuzi ya ZANU, yaani high command. Alishiriki katika kupanga mikakati na alikuwa mwanamke pekee kati ya wengine 27. Mbali na kuwa mwanachama wa idara ya wanawake ya ZANU, alichaguliwa pia kushika wadhifa katika kamati kuu ya shirika hilo.[5]

Tavarwisa alifariki dunia mnamo 3 Juni 1994.[6]

Alizikwa katika shamba la familia yake kijijini Gutu. Hakutambuliwa kama shujaa, jambo ambalo lilipelekea afisa wa mkoa wa ZANU-PF, Mapiye Wekwete, kumuuliza Makamu wa Rais marehemu Simon Muzenda kuhusu vigezo vya kutambua mashujaa wa mapambano ya mwanzo.

Wengi wa wenzake wa kiume ambao baadaye walijiunga na harakati za mapambano, na hata wale waliokuwa wamefundishwa na wanamke wa mapambano wa mwanzo kama Tavarwisa, walipatiwa heshima ya shujaa na kuzikwa katika Makaburi ya Taifa ya Mashujaa. [7]

  1. "Sheba Tavarwisa". Pindula (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2026-02-02.
  2. "womenafrica.com". forsale.godaddy.com. Iliwekwa mnamo 2026-02-02.
  3. Munyaradzi, Mawere; R, Mubaya, Tapuwa (2015-12-12). Colonial Heritage, Memory and Sustainability in Africa: Challenges, Opportunities and Prospects (kwa Kiingereza). Langaa RPCIG. ISBN 978-9956-763-72-6.{{cite book}}: CS1 maint: multiple names: authors list (link)
  4. Chung, Fay (2006). Re-living the Second Chimurenga: Memories from the Liberation Struggle in Zimbabwe (kwa Kiingereza). African Books Collective. ISBN 978-1-77922-046-2.
  5. Munyaradzi, Mawere; R, Mubaya, Tapuwa (2015-12-12). Colonial Heritage, Memory and Sustainability in Africa: Challenges, Opportunities and Prospects (kwa Kiingereza). Langaa RPCIG. ISBN 978-9956-763-72-6.{{cite book}}: CS1 maint: multiple names: authors list (link)
  6. "Sheba Tavarwisa". Pindula (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2026-02-02.
  7. Radio, Nehanda (2014-06-22), "Zanu PF not consistent on hero status – Nehanda Radio", Nehanda Radio (kwa American English), iliwekwa mnamo 2026-02-02