Seoul

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Majengo ya kihistoria na ya kisasa mjini Seoul

Seoul ni mji mkuu na mji mkubwa katika Korea ya Kusini. Kihistoria na hadi mwaka 1945 ilikuwa mji mkuu wa Korea yote.

Ina wakazi 10,276,968 kwenye eneo la km² 610.

Seoul iko kando ya mto Han katikati ya rasi ya Korea karibu na mpaka na Korea ya Kaskazini.

Jiji ni kitovu cha siasa, uchumi, utamaduni na elimu ya Korea Kusini.

Seoul ilikuwa mahali pa michezo ya olimpiki ya mwaka 1988.

Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Seoul kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.