Selemani Said Jafo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Seleman Jafo)
Mhe. Selemani Jafo Mb

Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi,Muungano na Mazingira
Aliingia ofisini 
2017
Rais John Magufuli

Mbunge wa Kisarawe
Aliingia ofisini 
2015

tarehe ya kuzaliwa 26 Mei 1973 (1973-05-26) (umri 50)
utaifa Mtanzania
chama CCM

Selemani Said Jafo (amezaliwa 26 Mei 1973) ni mwanasiasa Mtanzania na mwanachama wa Chama cha kisiasa cha Chama Cha Mapinduzi (CCM). Amechaguliwa kuwa mbunge wa Kisarawe kwa miaka 20152020. [1]

Mwaka 2017 alipewa cheo cha waziri katika Ofisi ya Rais kwa ajili ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)[2]. Mnamo tarehe 31 Machi 2021, aliteuliwa na raisi Mama Samia Suluhu Hassan kuwa waziri katika wizara ya ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na mazingira [3] Ameoa wake wanne (4) na wote wako hai.

Elimu[hariri | hariri chanzo]

Selemani Said Jafo alipata Elimu yake katika shule zifuatazo[4]

Mwaka wa kuanza Mwaka wa kumaliza Jina la shule Ngazi ya Elimu
2005 2007 Southern New Hampshire University Shahada ya Uzamili
1998 2001 Chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine Shahada ya kwanza
1995 1997 Shule ya Sekondari ya Minaki Elimu ya Sekondari
1991 1994 Shule ya Sekondari ya Maneromango Elimu ya Sekondari
1984 1990 Shule ya Msingi ya Kwala Elimu ya Msingi

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Tovuti ya Bunge la Tanzania, iliangaliwa Mei 2017
  2. "Profile | PO-RALG". www.tamisemi.go.tz (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-08-05. 
  3. https://www.dw.com/sw/mabadiliko-ya-baraza-la-mawaziri-tanzania/a-57066564
  4. "Profile | PO-RALG". www.tamisemi.go.tz (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-08-05.