Nenda kwa yaliyomo

Sanya Richards-Ross

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Sanya Richards-Ross (alizaliwa Februari 26, 1985) ni mwanariadha wa Marekani aliyestaafu, ambaye alishiriki mashindano ya kimataifa akiwakilisha Marekani katika mbio za mita 400. Mafanikio yake makuu katika mbio hizi ni pamoja na kuwa bingwa wa Olimpiki mwaka 2012, bingwa wa dunia mwaka 2009, mshindi wa medali ya shaba ya Olimpiki mwaka 2008, na mshindi wa medali ya fedha ya dunia mwaka 2005.[1] Kwa ushindi wake wa mwaka 2012, alikua mwanamke wa pili wa Marekani kushinda mbio za mita 400 katika Michezo ya Olimpiki na mwanamke wa kwanza wa Marekani kupata mataji mengi ya kimataifa katika mbio hizi. Katika umbali huu, Richards-Ross pia alikua bingwa wa kitaifa wa Marekani mara sita (2003, 2005, 2006, 2008, 2009, na 2012).[2][3]

  1. "Sanya Richards-Ross". worldathletics.org. World athletics federation.
  2. "Long ride 'worth the wait' as Richards-Ross claims elusive gold". World Athletics. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 10 Septemba 2021. Iliwekwa mnamo 10 Septemba 2021.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. "Felix takes on Richards-Ross over 400m in Eugene – IAAF Diamond League". World Athletics. Iliwekwa mnamo 10 Septemba 2021.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sanya Richards-Ross kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.