Samira Jassim
Samira Ahmed Jassim al-Azzawi au Samira Jassam (alizaliwa 1958)[1]anayejulikana pia kama Um al-Mumenin, "mama wa waumini", [2]inasemekana kuwa amefanya kazi na wanamgambo wa Sunni kutoka kundi la Ansar al-Sunnah katika mkoa wa Diyala.[3][4]
Jassim amekuwa kizuizini mikononi mwa vyombo vya usalama vya Iraq tangu tarehe 21 Januari 2009. Inadaiwa kwamba alikiri, kupitia video inayodaiwa kuwa ya mahojiano ya kukiri, kwamba alikuwa akiwatambua na kuwasajili watu walioweza kuwa washiriki wa mashambulizi ya kujitoa mhanga na pia kuwasaidia kuyatekeleza.
Zaidi ya hapo, katika mahojiano na shirika la habari la Associated Press, Jassim alieleza jinsi yeye na waasi walivyotumia ubakaji kama “silaha” ya kuwasajili wanawake kwenye mashambulizi ya kujitoa mhanga, ikidaiwa kuwa waathirika wa ubakaji waliokuwa wamedhalilishwa walishawishiwa kwamba wangeweza “kujiosha aibu” hiyo kwa kujitoa mhanga kwenye mashambulizi. [3][4]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Iraq Arrests Woman Tied to Bombings", New York Times, 3 February 2009
- ↑ "Iraqi woman had 80 women raped to recruit suicide bombers", Herald Sun, 4 February 2009
- 1 2 "Iraq's 'female bomber recruiter'", BBC News, 4 February 2009
- 1 2 "Woman set up rapes to 'recruit' 80 suicide bombers" Archived 2009-02-06 at the Wayback Machine, Canberra Times, 5 February 2009
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Samira Jassim kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |