Saka Acquaye

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Saka Acquaye (2 Novemba 192327 Februari 2007)[1] alikuwa mwanamuziki wa Ghana, mwandishi wa tamthilia, mchongaji sanamu na mbunifu wa nguo.

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Saka Acquaye alizaliwa Accra, tarehe 2 Novemba 1923, mtoto wa sita wa wazazi wake Regina na John Akweifio. Alisomea katika shule ya Methodist, shule ya kifalme ya Accra na kisha shule za wavulana za serikali. Alipata ufadhili wa Cadbury kuingia nyumba ya Cadbury, shule ya Achimota. Aliosha vyombo kwenye jumba la kulia la shule ili apate chakula cha ziada, kwa kuwa wazazi wake hawakuwa na uwezo wa kumudu kuongeza chakula chake. Akiwa chuoni alikua bingwa hurdler, akifanya mazoezi bila viatu na kutumia vizuizi vyake vya zamani vilivyotengenezwa na matawi ya miti. Akawa nahodha wa kikosi cha timu ya Taifa ya Wanariadha kuwakilisha Gold Coast mwaka wa 1950. Alikuwa Bingwa wa kuruka viunzi katika Gold Coast. Alipomaliza kozi yake huko Achimota, alifundisha kwa miaka kadhaa katika Chuo cha St. Augustine huko Cape Coast, mwanzoni mwa miaka ya 1950.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Nii Addokwei Moffatt, "Saka Acquaye Passes On", via Modern Ghana, 8 March 2007.
Makala hii kuhusu mambo ya muziki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Saka Acquaye kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.