Nenda kwa yaliyomo

Ripoti ya Mahakama ya Ringera ya mwaka 2003

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ripoti ya Mahakama ya Ringera ya mwaka 2003 ilikuwa ripoti ya Serikali ya Kenya iliyochapishwa na Kamati ya Uadilifu kupambana na rushwa Idara ya Mahakama nchini Kenya, kwa lengo la kutekeleza sera iliyojulikana kama upasuaji wa kina iliyoanzishwa na serikali mpya ya Rais Mwai Kibaki. Kamati hiyo ilikuwa chini ya uongozi wa Jaji Aaron Ringera.

Athari na matokeo ya baadaye

[hariri | hariri chanzo]

Kulingana na ripoti hiyo, majaji 5 kati ya 9 wa Mahakama ya Rufaa, majaji 18 kati ya 36 wa Mahakama Kuu na mahakimu 82 kati ya 254 walitajwa kuhusika na vitendo vya rushwa.[1] Wiki mbili ultimatum ama wajiuzulu au wafukuzwe kazi ilitolewa kwa majaji na mahakimu hao. Baadhi yao waliamua kujiuzulu au "kustaafu", huku wengine wakafungua mashauri ya kisheria kupinga kufukuzwa kwao. Mabaraza ya kusikiliza kesi hizo yakaanzishwa baadaye. Jaji Philip Waki alisafishwa (au aliachiliwa huru) mwishoni mwa mwaka 2004.

  1. Violette McCann. "Summary Of Issues To Be Highlighted In Icj Mission Report For Release To The Press - The Kenyan Section of the International Commission of Jurists". www.icj-kenya.org (kwa Kiingereza (Uingereza)). Iliwekwa mnamo 2025-07-30.