Regina Twala
Regina Gelana Twala (alizaliwa kama Regina Dorris Mazibuko; 1908–1968) alikuwa mwanaharakati wa haki za wanawake, mwandishi, mwalimu, mtafiti, mhubiri na kiongozi wa harakati za ukombozi nchini Afrika Kusini na Eswatini.
Twala alikuwa mtafiti na mwandishi mashuhuri pamoja na mwanaharakati wa kisiasa, na alishiriki kuanzisha Swaziland Progressive Party. Pia alikuwa mwanamke pekee aliyegombea kiti katika Baraza la Sheria la Swaziland mwaka 1963.
Wasifu
[hariri | hariri chanzo]Maisha ya awali
[hariri | hariri chanzo]Twala alizaliwa huko eNdaleni,[1] Afrika Kusini katika familia ya Wazulu.[2][3][4] . Alikulia katika kituo cha misheni ya Methodisti cha vijijini huko eNdaleni. Mama yake, Muriel Majozi, alifanya kazi kama mfanyakazi wa ndani mjini Durban.[5]
Elimu na kazi za awali
[hariri | hariri chanzo]Twala alihitimu kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Indaleni mwaka 1924, ambapo licha ya mipaka ya elimu ya misheni kwa wanawake wakati huo, alifaulu kitaaluma. Alipata mafunzo ya ualimu katika Adams College, shule ya wamisionari wa Marekani katika pwani ya Natal. Kazi yake ya kwanza ilikuwa kufundisha katika shule yake ya zamani ya Indaleni. Akiwa mwalimu mwanzoni mwa miaka ya 1930, Twala aliandika safu ya makala katika gazeti maarufu la kila siku la Waafrika Weusi Bantu World akitumia jina bandia la *Mademoiselle*. Mwanahistoria Joel Cabrita anaeleza kuwa safu 23 alizoandika zilikuwa “za kipekee katika kusherehekea uhuru wa wanawake kwa uwazi.” Mwaka 1935 alianza pia kuandika katika gazeti Umteteli wa Bantu kwa jina la kalamu *Sister Kollie*. Akiwa anaandika, alishinda mashindano kadhaa ya uandishi, ikiwemo nafasi ya pili ya tuzo ya May Esther Bedford kwa insha yake “Tales of Swazi and Hlubiland”.[5]
Johannesburg
[hariri | hariri chanzo]Mwaka 1936, Twala aliolewa na mume wake wa kwanza, Percy Kumalo, karani katika mgodi wa dhahabu mjini Johannesburg. Alihamia Johannesburg kuishi naye, na huko alifanya kazi katika shule ya misheni ya American Board, kinyume na desturi ya wakati huo iliyotarajia wanawake walioolewa kuacha kazi nje ya nyumbani.
Elimu ya juu
[hariri | hariri chanzo]Twala alisoma katika kundi la kwanza la Shule ya Jan Hofmeyr ya Kazi za Jamii, taasisi ya kwanza kufundisha wafanyakazi wa kijamii Weusi nchini Afrika Kusini, na alihitimu mwaka 1942 akiwa wa kwanza darasani.[5] Mwaka 1948, baada ya kumaliza shahada ya BA katika masomo ya kijamii, alikua mwanamke wa pili Mweusi kupata shahada kutoka University of the Witwatersrand huko Johannesburg (baada ya Mary Malahlela mwaka mmoja kabla).[6] Baadaye aliendelea na masomo ya uzamili, ambapo tasnifu yake ilihusu kazi za shanga za Kiafrika.[7][8]
Kazi
[hariri | hariri chanzo]Twala alikua mtafiti mwenye mchango mkubwa, hasa katika masuala ya wanawake na mila za Kiafrika Kusini.[9][6][10] Pia alianzisha maktaba maalum kwa matumizi ya wanawake.[6]
Kama mwandishi, alichangia makala katika magazeti mbalimbali nchini Swaziland, yakiwemo Umteteli Wa Bantu na Izwi lama Swazi.[6] Mara nyingi aliandika kwa kutumia majina bandia kama *Mademoiselle*, *Gelana*, *RD Twala*, *Reggie*, na *Sister Kollie*. Baada ya kifo chake, aliacha maandiko manne ya vitabu ambayo hayakuchapishwa.[6] Twala alikuwa mwanamke wa mwanzo katika harakati za ufeministi barani Afrika na kiongozi wa ukombozi aliyeshiriki katika harakati za kupinga ukoloni.[6]
Katika siasa, mwaka 1960 alishiriki kuanzisha Swaziland Progressive Party, ambapo alikuwa na ushawishi mkubwa.[6] Aligombea kiti katika Baraza la Sheria la Swaziland katika 1964 Swazi general election kama mgombea huru katika jimbo la Manzini. Alikuwa mwanamke pekee aliyeteuliwa katika uchaguzi huo, lakini hakushinda kiti. Aidha, Twala alikuwa mmoja wa waanzilishi wa ibada ya Pentekoste katika eneo hilo na mshiriki hai wa harakati za Ukristo wa kiinjili.[6] Anatajwa kuwa alisaidia kuanzisha dhehebu la Assemblies of God katika eneo la sasa la eSwatini.
Maisha binafsi
[hariri | hariri chanzo]Mwaka 1939, aliolewa na mwanaharakati mwenzake Dan Twala, ambaye alishirikiana naye kwa karibu katika kazi zake.[11] Wanandoa hao walikuwa marafiki wa karibu na Nelson Mandela pamoja na Winnie Madikizela-Mandela.[6]
Twala alifariki mwaka 1968, mwezi mmoja kabla ya Swaziland kupata uhuru.[6]
Urithi
[hariri | hariri chanzo]Kitabu cha Joel Marie Cabrita kuhusu Twala kiitwacho Written Out: The Silencing of Regina Gelana Twala, kilichapishwa Januari 2023 na Ohio University Press pamoja na Wits University Press[12]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Cabrita, Joel (2023). Written Out: The Silencing of Regina Gelana Twala. Johannesburg: Wits University Press. ISBN 978-1-77614-861-5.
- ↑ "A Virtual Summer: CESTA 2020 Research Anthology" (PDF). Center for Spatial and Textual Analysis (CESTA) at Stanford University. 2020. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo (PDF) mnamo 2021-01-30. Iliwekwa mnamo 2021-01-28.
- ↑ "Love Letters in Beads". The Times-Tribune. 1954-04-26.
- ↑ INS (1954-03-15). "African Girls Sent Boy Friends Love Letters In Varied Forms of Bead Talk". Palladium-Item.
- 1 2 3 Cabrita, Joel (2023). Written Out: The Silencing of Regina Gelana Twala. Johannesburg: Wits University Press. ISBN 978-1-77614-861-5.
- 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Feder, Sandra (2020-02-24). ["Stanford historian's high school research transformed her life". Stanford) News (kwa Kiingereza).
{{cite web}}: Check|url=value (help) - ↑ Hitilafu ya kutaja: Invalid
<ref>tag; no text was provided for refs named:3 - ↑ Reynolds, Pamela (1989). Childhood in Crossroads: Cognition and Society in South Africa. Cape Town: D. Philip. ISBN 0-86486-117-6. OCLC 21385348.
- ↑ INS (1954-03-15). "African Girls Sent Boy Friends Love Letters In Varied Forms of Bead Talk". Palladium-Item.
- ↑ Washburn, Dorothy Koster; Donald W. Crowe (2004). Symmetry comes of age : the role of pattern in culture. Seattle: University of Washington Press. ISBN 0-295-98366-3. OCLC 52418067.
- ↑ Erlmann, Veit. (1996). Nightsong : performance, power, and practice in South Africa. University of Chicago Press. ISBN 0-226-21720-5.
- ↑ "Written Out: The Silencing of Regina Gelana Twala". Ohio University Press. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2023-01-31. Iliwekwa mnamo 2023-01-30.