Raymunda Torres y Quiroga
Mandhari

Raymunda Torres y Quiroga alikuwa mwandishi na mwanaharakati wa haki za wanawake kutoka nchini Argentina. Alitetea upatikanaji wa elimu na ukombozi wa wanawake nchini Argentina.[1]
Wasifu
[hariri | hariri chanzo]Raymunda Torres y Quiroga alizaliwa katika mkoa wa Entre Ríos nchini Argentina. Taarifa nyingi za maisha yake hazijulikani.
Mara nyingi alitumia majina ya kalamu (Majina ya kubuni) kuandika makala zake.Alichapisha hadithi zilizobeba mawazo yake kuhusu ukombozi wa wanawake na pia alizungumzia mada ya mauaji ya wanawake.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Raimunda Torres y Quiroga: una desconocida autora de literatura fantástica en la Argentina del siglo XIX". Brumal. Iliwekwa mnamo 16 Machi 2026.