Nenda kwa yaliyomo

Rania Hussein Amin

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Rania Hussein Amin (alizaliwa 1965) ni mwandishi na mchoraji wa vitabu vya watoto kutoka Misri. Anajulikana zaidi kupitia mfululizo wa vitabu vya Farhana, ambavyo yeye mwenyewe ndiye aliyekuwa akiandika na kuchora picha zake.[1]

Michoro na maandishi yake yamechapishwa katika majarida ya “Nos El Donia” na “Qatar Al Nada”. Mbali na hilo, ameandika zaidi ya vitabu 45 vya watoto na pia amechora vielelezo vya vitabu vilivyoandikwa na waandishi mashuhuri, ikiwemo kitabu “Me and I” cha Michel Hanna.[2]

Katika safari yake ya kazi, Rania Amin pia amekuwa na mchango mkubwa katika elimu, hususan katika kusaidia watoto wenye mahitaji maalum. Kupitia vitabu vyake na mhusika wa Farhana aliyemuunda, amekuwa akihamasisha na kuelimisha wazazi kuhusu mbinu bora na maadili ya malezi ya watoto.

  1. "رانية أمين", ويكيبيديا (kwa Kiarabu), 2020-08-24, iliwekwa mnamo 2021-02-28
  2. مقدمة, مقدمة العدد (2021-02-01). "مقدمة العدد الأول 232 فبراير". مجلة القراءة والمعرفة. 21 (1): 1–14. doi:10.21608/mrk.2021.148905. ISSN 2735-3273.
Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Rania Hussein Amin kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.