Ramzan Khadzhiev
Ramzan Khadzhiev (Kirusi: Хаджиев Рамзан; 14 Novemba 1955 – 11 Agosti 1996) alikuwa mkuu wa ofisi ya eneo la Kaukazi ya Kaskazini ya Televisheni ya Umma ya Urusi (ORT). Khadzhiev alikuwa mwandishi wa habari wa 19 kuuawa ndani ya kipindi cha miezi 20 ya Vita ya Kwanza ya Chechnya.[1]
Mnamo tarehe 11 Agosti 1996, Khadzhiev aliuawa alipokuwa akijaribu kuondoka Grozny, mji mkuu uliokuwa vitani wa Chechnya, kwa gari pamoja na mke wake na mtoto mdogo. Alipigwa risasi kichwani baada ya kupita katika kituo cha ukaguzi cha jeshi la Urusi.[2] ORT iliripoti kwamba waasi wa Chechnya walimlenga Khadzhiev, ambaye alikuwa Mchechen kwa asili, kwa sababu aliunga mkono serikali iliyowekwa na Moscow. Hata hivyo, abiria aliyekuwa kwenye gari lao aliieleza televisheni ya NTV ya Urusi kwamba walishambuliwa na gari za kivita za Urusi.[3]
Baadaye, wenzake walithibitisha kwamba alipigwa risasi kichwani mara mbili na askari wa hirikisho la Urusi.[4] Hakukuwa na uchunguzi ulioanzishwa, na ORT haikuwahi kufuatilia uchunguzi wa umma.[5]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Russian, Chechen leaders OK cease-fire Archived 2007-10-16 at the Wayback Machine, Associated Press
- ↑ Journalist killed in Chechnya p.25 Archived 2011-06-04 at the Wayback Machine, Editor & Publisher
- ↑ It's a Dangerous Job: 26 Journalists Were Murdered in 1996 Archived 2006-02-11 at the Wayback Machine, Columbia Journalist Review
- ↑ No. 157, Part I, 14 August 1996 RFE/RL Archive, Radio Free Europe
- ↑ Russia's Harsh Press Climate by Catherine A. Fitzpatrick Archived 2012-12-05 at the Wayback Machine, Committee to Protect Journalists
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ramzan Khadzhiev kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |