Q Moses
Qaeqaho Moses Maraamele (aliyezaliwa mwaka 1973 huko Dekar, Wilaya ya Ghanzi), anayejulikana pia kama Q Moses ni msanii wa sanaa ya kuona na mtengenezaji wa chapa aliyejifunza mwenyewe kutoka Botswana. Yeye ni mwanachama wa jamii ya San, kundi la asili la Afrika ya Kusini. Kazi zake zinaangazia zaidi uhifadhi na uendelezaji wa urithi wa kitamaduni wa San kupitia sanaa.[1]
Maisha ya awali na elimu
[hariri | hariri chanzo]Maraamele alilelewa Dekar, ambapo alizungukwa na mila pamoja na mandhari ya Jangwa la Kalahari.[2] Jina lake, Qãetcao linalomaanisha moyo mwema alipewa na marafiki zake wa utotoni kutoka jamii ya San likionyesha uhusiano wake wa kina na jamii pamoja na utamaduni wake.[3] Alianza safari yake ya kisanaa mwaka 1994 kwa kujiunga na Mradi wa Sanaa wa Kuru, jukwaa linalounga mkono wasanii wa asili nchini Botswana.[4]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "MOSES MAARAMELA". Kuona Trust | Centre For Visual Arts In Kenya (kwa American English). 2019-08-16. Iliwekwa mnamo 2025-10-03.[dead link]
- ↑ "Qaeqhao Moses Biography". CreativeTswana.
- ↑ "About Kuru Art - Kuru Art Project" (kwa American English). 2023-04-03. Iliwekwa mnamo 2025-10-03.
- ↑ "Artist QAEQHAO MOSES". The Cape Gallery. Iliwekwa mnamo 2025-10-03.
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Q Moses kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |