Plato

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya kichwa cha Plato.

Plato (kwa Kigiriki: Πλάτων, Platon; 427 KK - 347 KK) alikuwa kati ya wanafalsafa muhimu zaidi wa Ugiriki ya Kale, akiwa mwanafunzi wa Sokrates na mwalimu wa Aristoteles.

Alibuni mawazo mengi yenye maana hadi leo. Wanafalsafa wa kisasa wamesema ya kwamba falsafa yote inamtegemea Plato.

Aliandika mafundisho yake kwa umbo la majadiliano - yaani watu wawili au zaidi wanajadili mawazo wakikubaliana au kutokubaliana nayo. Kwa njia hiyo Plato alipenda kueleza fikra zake.

Mara nyingi Sokrates ni msemaji mkuu katika majadiliano ya Plato. Huonyeshwa akiwauliza watu juu ya yale wanayoyaamini akiendelea kuuliza maswali kama mawazo yao yanalingana na mantiki. Haieleweki ni kiasi gani Plato alitumia kweli mafundisho ya Sokrates mwenyewe au kama alimtumia zaidi kifasihi kama mhusika akieleza fikra zake Plato kupitia mdomo wa Sokrates wa majadiliano.

Kati ya maandiko muhimu zaidi ya Plato ni "Politeia" yaani "kuhusu dola".

Dhana na vitu[hariri | hariri chanzo]

Katika falsafa ya Plato kuna tofauti muhimu kati ya dhana na kitu. Dunia ya kweli ni dunia ya dhana.

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Plato kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.