Peya Mushelenga
Samuel Abraham Peyavali "Peya" Mushelenga (amezaliwa Oshigambo, Ovamboland, 1 Septemba 1975) ni mwanasiasa na mshairi wa Namibia. Ameelimika kwa upana, akiwa na sifa za kitaaluma kumi na tano kutoka vyuo vikuu saba tofauti.
Mwanachama wa SWAPO, Mushelenga alikuwa Mbunge wa Bunge la Taifa la Namibia kuanzia 2005 hadi 20 Machi, 2025. Amewahi kuhudumu katika Baza la Mawaziri la Namibia katika wizara mbalimbali na mara ya mwisho aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano kuanzia 9 Februari, 2024 hadi 21 Machi, 2025.
Maisha ya awali na elimu
[hariri | hariri chanzo]Peya Mushelenga alizaliwa Oshigambo katika Mkoa wa Oshikoto, kaskazini mwa Namibia. Alisoma katika Shule ya Sekondari ya Juu ya Oluno hadi mwaka 1992 na kisha akaingia katika Chuo Kikuu cha Namibia (UNAM).
Mushelenga amekusanya digrii kumi na tano za vyuo vikuu katika maisha yake ya kitaaluma; gazeti la New Era (Namibia) lilimuita "msomi mwenye hamu zaidi nchini Namibia".[1][2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Kangira, Jairos (4 Aprili 2022). "Mushelenga graduates with second PhD". New Era.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Mushelenga, Peya". Parliament of Namibia. Iliwekwa mnamo 28 Aprili 2018.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Peya Mushelenga kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |