Nenda kwa yaliyomo

Vifaa vya pembe za ndovu vya Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Pembe za ndovu za Afrika)

Vifaa vya pembe za ndovu vya Afrika ni vitu na vifaa vilivyotengenezwa kwa pembe za ndovu au vinavyojumuisha nyenzo ya ndovu inayotokana na bara la Afrika. Pembe za ndovu kutoka Afrika zilianza kutafutwa sana kufikia karne ya 14, kwa kiasi fulani kutokana na ubora hafifu wa Pembe za ndovu za Asia.[1] Wakati pembe za ndovu za Asia ni mepesi kuvunjika, magumu zaidi kuyasugua ili yang'ae na huwa na mwelekeo wa kugeuka rangi kuwa ya manjano yanapopata hewa, pembe za ndovu za Afrika mara nyingi hupatikana katika vipande vikubwa zaidi, yana rangi ya maziwa inayotafutwa zaidi na ni rahisi zaidi kuyachonga. Pembe za ndovu kutoka Afrika zilitoka katika aina mbili za tembo barani Afrika tembo wa nyika anayependwa zaidi mwenye pembe kubwa na nzito au tembo wa msitu mwenye pembe ndogo na wima.

Pembe za ndovu pamoja na vitu vya ndovu kama vile barakoa, vyombo vya chumvi, olifanti na alama nyingine za umuhimu vimekuwa vikibadilishana na kutumika kama zawadi na katika sherehe za kidini kwa mamia ya miaka barani Afrika.[2][3][4][5][6]

  1. Sheriff, A. (2002). Slaves, Spices, & Ivory in Zanzibar: Integration of an East African commercial empire into the World Economy, 1770-1873. J. Currey.
  2. Doty, Lewis (2022-11-11). "History of the ivory trade with special reference to Africa - Elephant Populations". Ecology Center (kwa Kiingereza). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2022-11-21. Iliwekwa mnamo 2022-11-21.
  3. Sheriff, A. (2002). Slaves, Spices, & Ivory in Zanzibar: Integration of an East African commercial empire into the World Economy, 1770-1873. J. Currey.
  4. Siegmann, William; Adand, Joseph C. E.; Dumouchelle, Kevin D. (2009). Iliandikwa kwenye Brooklyn, NY. African Art: A Century at the Brooklyn Museum. Brooklyn, NY, Munich: Brooklyn Museum and DelMonico Books/Prestel. ISBN 978-3-7913-4321-1. OCLC 316514906.
  5. Rosenthal, Ricky (1971). The Sign of the Ivory Horn: Eastern African Civilizations. Dobbs Ferry, N.Y: Oceana Publications. ISBN 9780379004496. OCLC 206749.
  6. Ross, Doran H. (1992). Elephant: The Animal and its Ivory in African Culture. Los Angeles: Fowler Museum of Cultural History, University of California, Los Angeles. ISBN 0-930741-25-0. OCLC 27035844.
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vifaa vya pembe za ndovu vya Afrika kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.