Nenda kwa yaliyomo

Ousmane Dembele

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ousmane Dembele (2015)

Ousmane Dembélé (alizaliwa 15 Mei 1997) ni mchezaji wa soka wa Ufaransa ambaye anachezea klabu ya Barcelona F.C. na timu ya kitaifa ya Ufaransa.

Dembélé alianza kazi yake ya soka huko Rennes kabla ya kujiunga na klabu ya Dortmund mwaka 2016. Mwaka mmoja baadaye, alihamia Barcelona kwa ada ya awali ya milioni 105.

Borussia Dortmund

[hariri | hariri chanzo]

Baada ya kushinda Vikombe 20 na kufunga magoli matano katika ngazi ya vijana, Dembélé alipandishwa kwenda ligi daraja la kwanza mwaka 2016 na klabu ya Borussia Dortmund.

Mnamo Mei 12, 2016, Dembélé alisaini mkataba wa miaka mitano na klabu ya Ujerumani Borussia Dortmund. Mnamo tarehe 14 Agosti 2016, Dembélé alianza kucheza na kushinda 2-0 dhidi ya Bayern Munich katika DFL-Supercup.

FC Barcelona

[hariri | hariri chanzo]

Tarehe 25 Agosti 2017, FC Barcelona ya La Liga ilitangaza kuwa wamefikia makubaliano ya kutia saini kwamba wanataka kumnunua Dembélé kwa € milioni 105 pamoja na kuongeza milioni 40 za ziada.

Ousman dembele alicheza mechi yake ya kwanza akiwa na Barcelona dhidi ya Espanyol ambapo aliotokea benchi na kutoa assisting kwa Luis Suarez Barcelona wakishindi 4-0. Alicheza tena mechi yake ya pili dhidi ya Juventus katika klabu bingwa Ulaya. Mechi yake ya tatu ilikuwa dhidi ya Granada ambapo aliumia na kukaa nje kwa myezi minne.

Alirudi Desemba 2017 kwenye mechi dhidi ya Celta Vigo kwenye kombe la mfalme.

Bao lake la kwanza alifunga dhidi ya Chelsea kwenye ligi ya mabingwa Ulaya. Bao lake la kwanza kwenye La Liga alifunga dhidi ya Celta Vigo kwenye sare ya 2-2.

Msimu wa 2025–26

[hariri | hariri chanzo]

Tarehe 13 Agosti 2025, Dembélé alishinda UEFA Super Cup na Paris Saint-Germain, akifunga katika ushindi wa penalti 4–3 baada ya sare ya 2–2 dhidi ya Tottenham Hotspur. Pasi yake ya dakika za nyongeza iliyomsaidia Gonçalo Ramos kufunga kwa kichwa na mkwaju wake wa penalti uliyoingia wakati wa mikwaju ya penalti vilikuwa miongoni mwa mchango wake uliomfanya apewe tuzo ya Mchezaji Bora wa Mechi.[1] Tarehe 30 Agosti 2025, Dembélé alifunga magoli yake mawili ya kwanza ya msimu, yote kwa njia ya penalti katika ushindi wa ugenini wa 6–3 dhidi ya Toulouse.[2] Akiwa na timu ya taifa mapema Septemba 2025, Dembélé alipata jeraha la msuli wa paja (hamstring) lililomweka nje ya uwanja kwa muda wa wiki sita.[3] Mwezi huohuo, alishinda Tuzo ya Ballon d'Or ya 2025.[4]

  1. "Ousmane Dembélé named 2025 UEFA Super Cup Player of the Match". UEFA. 13 Agosti 2025. Iliwekwa mnamo 13 Agosti 2025.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. "João Neves and Paris put on a show at the Stadium!". www.psg.fr (kwa Kiingereza). 2025-08-30. Iliwekwa mnamo 2025-08-30.
  3. "Source: PSG irate over Dembélé injury with France". ESPN.com (kwa Kiingereza). 2025-09-06. Iliwekwa mnamo 2025-09-10.
  4. "Ballon d'Or 2025 LIVE: Winners, times & updates from ceremony in Paris". BBC Sport (kwa Kiingereza (Uingereza)). Iliwekwa mnamo 2025-09-22.
Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ousmane Dembele kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.