Kanisa Katoliki nchini Ufilipino
Mandhari
(Elekezwa kutoka Orodha ya makadinali wa Ufilipino)
Kanisa Katoliki nchini Ufilipino ndiyo madhehebu makubwa zaidi ya kidini nchini humo na lina idadi kubwa ya Wakatoliki kuliko karibu zote duniani.
Imani ya Kikatoliki ililetwa nchini Ufilipino na wamisionari kutoka Uhispania katika karne ya 16.
Takriban miaka 400 baadaye, mnamo mwaka 1960, Rufino J. Santos, Askofu Mkuu wa Manila, akawa Mfilipino wa kwanza kuwa kardinali. Tangu wakati huo, jumla ya Wafilipino kumi wameinuliwa katika hadhi ya kardinali.
Mnamo Mei 1, 2020, Luis Antonio G. Tagle, Pro-Prefekti wa Sehemu ya Uinjilishaji wa Kwanza katika Idara ya Uinjilishaji, alipandishwa kuwa kardinali-askofu. Yeye ndiye Mfilipino wa kwanza kushika cheo cha juu zaidi cha kardinali katika Kanisa Katoliki.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Pope Francis promotes Cardinal Tagle to rank of Cardinal-Bishop". CNN Philippines. 1 Mei 2020. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo Juni 24, 2021. Iliwekwa mnamo 21 Juni 2021.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kanisa Katoliki nchini Ufilipino kama historia yake au maelezo zaidi? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |