Nenda kwa yaliyomo

Nyiva Mwendwa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Winfred Nyiva Mwendwa ni mwanasiasa wa Kenya. Alikuwa mwanamke wa kwanza wa Kenya kuhudumu kama waziri wa baraza la mawaziri.

Maisha ya awali na elimu

[hariri | hariri chanzo]

Alisoma katika Alliance Girls High School,[1] na alikuwa miongoni mwa walimu wa kwanza Waafrika kiasili kufundisha katika The Kenya High School katikati ya miaka ya 1960, akifundisha masomo ya sayansi ya nyumbani (Domestic Science). Alichaguliwa kuwa Mbunge wa Kitui West Constituency mara tatu: mwaka 1974 na 1992 akiwania kupitia Kenya African National Union (KANU), na mwaka 2002 kupitia National Rainbow Coalition (NARC).

Katika uchaguzi wa mwaka 2007, aligombea kiti hicho kupitia ODM-Kenya lakini alishindwa na Charles Mutisya Nyamai. Mwaka 2013, alichaguliwa kuwa mwakilishi wa kwanza wa wanawake wa Kitui County katika uchaguzi wa ndani wa Kaunti ya Kitui, akigombea kwa tiketi ya Wiper Democratic Movement-Kenya (WDM-K). Mwaka 2016, alitangaza nia yake ya kustaafu siasa za ushindani baada ya miaka 40 tangu aanze safari yake ya kisiasa.[2][3]

  1. Center for Multiparty Democracy: Politics and Parliamentarians in Kenya 1944–2007 Archived 2008-10-28 at the Wayback Machine
  2. "Parliamentary election results 2007 - Kitui West". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2008-03-02. Iliwekwa mnamo 9 Julai 2017.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. "Woman of firsts and style". Iliwekwa mnamo 9 Julai 2017.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nyiva Mwendwa kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.