Ntlhoi Motsamai
Ntlhoi Motsamai (amezaliwa 1963) ni mwanasiasa wa Lesotho ambaye aliwahi kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa wa Spika wa Bunge la Taifa la Lesotho kuanzia 1999 hadi 2012. Alichaguliwa tena kuanzia Machi 2015 hadi Juni 2017. Motsamai alifanya kazi kama mwalimu kabla ya kuingia kwenye siasa.
Maisha ya Awali
[hariri | hariri chanzo]Motsamai alizaliwa katika kijiji cha mbali cha Ha Pafoli, kilichopo Wilaya ya Mohale's Hoek. Alisoma katika Shule ya Sekondari ya Eagle's Peak na baadaye akasomea katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Lesotho, ambako alihitimu shahada ya Sayansi ya Elimu (B.Sc.Ed.) akiwa na masomo ya msingi ya baiolojia na kemia. Baada ya kuhitimu, Motsamai alianza kufundisha katika Shule ya Sekondari ya St. John huko Mafeteng. Baadaye alirudi katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Lesotho ili kukamilisha shahada ya Uzamili wa Elimu (M.Ed.) huku akifanya kazi katika ofisi ya dean.[1][2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Rosenberg, Scott; Weisfelder, Richard (2013). Historical Dictionary of Lesotho. Scarecrow Press. uk. 392. ISBN 978-0810879829.
- ↑ "Ntlhoi Motsamai elected new Lesotho National Assembly Speaker" Archived 19 Oktoba 2016 at the Wayback Machine, SABC News, 10 March 2015. Retrieved 17 October 2016.
| Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ntlhoi Motsamai kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |