Nonini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nonini (amezaliwa 1 Oktoba 1982) jina lake haswa ni Hubert Nakitare, ni msanii wa nyimbo aina ya hip hop kutoka nchini kenya awali akisajiliwa na calif records,lakini baadaye alijiunga na homeboyz productions. Yeye alijitosa kwenye ulingo wa muziki wa mijini nchini Kenya kupitia wimbo wake "Nonini ni Nani?" kupanda kwa umaarufu wake kitaifa na kikanda haukuanza hata hivyo mpaka alipotowa wimbo wake "Manzi wa Nairobi" mwaka 2002, wimbo ambao ulisifu uzuri wa wanawake wa Kenya na kufuatiliwa na wimbo "Weh Kamu". Yeye aliendelia kwa kutoa albamu yake "Hanyaring game" mwishoni mwa mwaka wa 2004 ambayo ilihusisha wimbo maarufu "Keroro" neno la kisheng lenye maana ya pombe ya bia.Nonini anajulikana kwa kutoa wimbo wa kwanza wa Genge

mapema katika kazi yake ya uimbaji.

Baadaye,wimbo Nani mwenza, kwa ushirikiano na mwanamuziki kutoka Tanzania Juma Nature, uliweza kujulikana kikanda. Katika ubunifu mkubwa hivi karibuni,ameshirikiana pamoja na msanii Nameless kuunda wimbo wa kitaifa wa Ijumaa ujulikanao kama "furahi day" ambao umechezwa sana katika vituo vya utangazaji. nyimbo zote mbili ziko kwenye albamu yake ya pili Mwisho Ya Mawazo,iliyotolewa mwaka 2007. Albamu yake iliwahusisha wanamuziki wakiwemo Nyota Ndogo, Mercy Myra, Profesa Jay na Q-Chief Agosti 2007, Nonini alikuwa miongoni mwa Wakenya 100 wenye ushawishi mkubwa kama ilivyochanguliwa na gazeti la The Standard Nonini alishinda tuzo bora la kimuziki la Chaguo La Teeniez mwaka 2008 kwa video yake ya "Mtoto Mzuri" katika Mwaka wa 2009 alitajwa kama Balozi wa international Lifestyle na Chuo Kikuu cha Limkokwing nchini Malaysia

Nonini ni chotara nusu mluhya na nusu mKamba.

Leo Sun Nonini ina mipaka mipaka unimaginable kuliko mtu ambaye anaongea kwenye ukurasa huu. Kuangalia kwa hilo.

P-Unit[hariri | hariri chanzo]

hivi karibuni alianza kikundi kipya kinachojulikana kama P-Unit (pro habo unit ) kinacho wahusisha waimbaji Bonnie, Frasha, Gabu na yeye mwenyewe. kikundi cha p-unit kimetoa baadhi ya nyimbo  hasa cha  "Si lazima" .  "Si lazima" ni wimbo unaozungumzia wakati wa uhusiano  ambapo wanandoa hawahitaji  kufanya ngono wanaweza kwenda nyumbani na kutofanya mapenzi.Watu wametambua suala la kejeli katika ujumbe wake na nyimbo alizocheza hapo awali. katika mwaka wa 2007 kwenye tuzo la kimuziki cha Kisima P-Unit ilishinda kwenye kitengo cha tuzo la Kikundi cha boomba  Kwa Nonini, ilikuwa ni mara ya kwanza yeye kushinda tuzo la Kisima licha ya kuwa hewani kwa miaka mingi. wimbo wao wa pili ulijulikana kama Kushoto-Kulia;   nyimbo zote mbili ziko kwenye albamu yake ya Mwisho ya Mawazo.  P-Unit ilishinda katika kundi bora kwenye Chaguo La Teeniez mwaka wa 2007 na 2008  na kundi hilo liliteuliwa kwa uzinduzi wa tuzo la (mwaka 2008) MTV Africa Music  Wakati wa tuzo la mziki la Kisima P-Unit ilishinda katika kitengo cha Kikundi  jamii cha boomba , vilevile pamoja na mwanamziki DNA kutokana na Ushirikiano wao kwa wimbo wa "Una"

Marejeleo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]