Nollywood

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nollywood ni jina la kutaja filamu ambazo zinatengenezwa, kusambazwa, na kuigizwa na watu wa Nigeria. Soko hili la filamu za Nigeria lilianza kukua kwa haraka zaidi kunako miaka ya 1990 na 2000 na kuifanya iwe nchi ya pili duniani kwa ukubwa wa soko la filamu, kwa matokeo ya idadi ya filamu zinazozalishwa kwa mwaka. Hii ni kabla ya soko la filamu la Marekani na India.[1] Kwa mujibu wa Hala Gorani na Jeff Koinange wafanyakazi wa zamani wa CNN, soko la filamu la Nigeria lina dola za Kimarekani takribn milioni 250, wakichanganya baadihi ya video 200 ambazo zilimetengenezwa kwa ajili ya soko la ndani kila mwezi.[2][3] Kwa kufuatiwa matangazo yalirushwa na kipindi cha Kimarekani kinachotangazwa na Oprah Winfrey, alitangaza kwamba soko la filamu la Nigeria limepita thamani ya bilioni 2.3 za Kimarekani kwa mwaka wa 2008.

Mandhari[hariri | hariri chanzo]

Filamu nyingi za Nollywood zina mandhari ambayo yanahusu maadili na hali ya utata unaowakumba Waafrika wa sasa. Kuna baadhi ya filamu zinapromoti imani za Ukristo au Uislamu, na kuna baadhi ya filamu, yaani, hazifichi kitu zinataja dhahili masuala ya injili. Nyinginezo, lakini, hushughulikia maswali ya utofauti wa kidini, kama vile ile filamu maarufu ya One God One Nation, inahusu mwanaume wa Kiislamu na mwanamke wa Kikristo ambao wanataka kuoana lakini wanapitia vikwazo vingi sana.

Waigizaji mashuhuri[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Nigeria surpasses Hollywood as world's second largest film producer – UN. United Nations (2009-05-05). Jalada kutoka ya awali juu ya 2011-08-14. Iliwekwa mnamo 2009-09-30.
  2. The Best of African Film in 2004. CNN (2004-12-18). Iliwekwa mnamo 2008-10-09.
  3. Freeman, Colin (2007-05-07). In Nollywood, 'lights, camera, action' is best case scenario. Daily Telegraph. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-02-15. Iliwekwa mnamo 2008-10-09.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu filamu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nollywood kama waigizaji wake, hadithi au matoleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.