Nenda kwa yaliyomo

Ngongo ya Chintu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ngongo ya Chintu, anayejulikana kama Mwalimu wa Buli (karne ya 19), alikuwa mchongaji wa Sanaa ya Luba katika eneo ambalo leo ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.[1] Mengi hayajulikani kuhusu maisha yake, lakini kazi zake zimekusanywa kimataifa na inasemekana kuwa aliheshimiwa sana katika kijiji chake cha nyumbani.

Maisha na Kazi

[hariri | hariri chanzo]
Sanamu ya Caryatid na Ngongo ya Chintu

Ngongo ya Chintu (cheo cha heshima kinachomaanisha "chui mkuu, baba wa vitu vilivyochongwa")[1] alifanya kazi katika kile kilichokuwa Ufalme wa Luba, wakati fulani kati ya mwaka 1810 na 1870.[1] Alendelea na utamaduni mrefu wa sanaa ya Hemba. Vinyago vya Hemba mara nyingi viliheshimu viongozi mashuhuri wa kiume wa kabila. Ngongo ya Chintu alichonga sanamu za mababu pamoja na sanamu za wanawake kama vile vyombo na caryatids, ambazo zilitumika kama viti kwa viongozi.[2][3][4]

  1. 1 2 3 LaGamma, Alisa (2011). Heroic Africans: Legendary Leaders, Iconic Sculptures, Metropolitan Museum of Art publications, New York. ISBN 1588394328.
  2. Marilyn Stokstad (Agosti 2009). Art History, Volume One. Pearson Education Canada. ISBN 978-0-205-74835-8.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. Stool (a) with kneeling female figure
  4. Prestige Stool: Female Caryatid
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ngongo ya Chintu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.