Nenda kwa yaliyomo

Nara Smith

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nara Aziza Smith (alizaliwa 27 Septemba, 2001) ni mwanamitindo na mshawishi wa mitandao ya kijamii mwenye asili ya Afrika Kusini na uraia wa Ujerumani, anayeishi Marekani. Anajulikana zaidi kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii kwa video fupi za upishi, ambapo huandaa vyakula kutoka mwanzo kabisa akiwa amevalia mavazi ya kifahari, huku akisimulia kwa sauti ya chini na tulivu.[1][2]

Maisha ya awali

[hariri | hariri chanzo]

Nara Aziza Pellmann alizaliwa tarehe 27 Septemba 2001 huko Bloemfontein, Afrika Kusini, akiwa mtoto wa mama mwenye asili ya Mosotho na baba Mjerumani. Alipokuwa bado mchanga, familia yake ilihamia Frankfurt, Ujerumani, ambako alikulia na kutumia sehemu kubwa ya utoto wake.

Kupitia video aliyochapisha kwenye TikTok, Nara ameeleza kuwa Kiingereza na Kijerumani ni lugha zake za kwanza (lugha mama). Ana ndugu wawili wadogo, kaka mmoja na dada mmoja, pamoja na kaka wa kambo upande wa mama yake.[3]

  1. McCall, Tyler (15 Desemba 2015). "50 Models Have Been Scouted With This Hashtag and You Could Be Next". Teen Vogue.{{cite magazine}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. Mowatt, Robyn (20 Agosti 2024). "Nara Aziza Smith The Stylish Foodie And Muse Is The Face Of Aritzia's Sweatfleece New Campaign". Iliwekwa mnamo 2 Machi 2025.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. Butler, Sinead (2 Mei 2024). "Who is Nara Smith and why are her recipes going viral?". Iliwekwa mnamo 13 Mei 2024.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nara Smith kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.