Naomi Jacobson

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Naomi Jacobson alikuwa mchongaji. Alizaliwa Windhoek Kusini Magharibi mwa Afrika mnamo 1 Juni 1925. [1] Baba yake alikuwa Israel Goldblatt, mwanasheria na mfuasi wa uhuru wa Namibia. [1] Alisoma katika Chuo Kikuu cha Cape Town ambapo alikutana na kuolewa na mume wake Larry. Walihamia Johannesburg mwaka 1973. [1] Kipindi cha kazi yake alitengeneza sanamu za watu mbalimbali akiwemo Lord Baden-Powell, Nelson Mandela, Oliver Tambo, wafalme wa Kizulu Shaka na Cetshwayo, Steve Biko, na Sir Seretse Khama . [1] Alifariki mnamo mwaka 2016. [1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 1.2 1.3 1.4 Saks, David. "Top sculptress Naomi Jacobson dies age 91", South African Jewish Report, 1 June 2016. Retrieved on 19 August 2017. Archived from the original on 2019-12-14. 
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Naomi Jacobson kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.