Namba za Kiroma
Namba za Kiroma nu mfumo wa namba jinsi ulivyokuwa kawaida wakati wa Roma ya Kale na katika mwandiko wa Kilatini. Mfumo huu unaendelea kutumiwa hadi leo kwa namba za pekee hasa katika muundo wa orodha ambako mgawanyo ni wa ngazi mbalimbali. Ni kawaida kwa kutofautisha watu wenye jina lilelile kwa mfano wafalme au mapapa: Papa Benedikto XVI (=wa 16) au Malkia Elizabeth II (=wa pili).
Yaliyomo
Herufi za alfabeti kama alama za namba[hariri | hariri chanzo]
Jinsi ilivyo katika lugha mbalimbali hata Waroma walitumia herufi za alfabeti ya Kilatini pia kwa matumizi kama alama za namba.
Alama za kimsingi[hariri | hariri chanzo]
Herufi chache zilitumiwa kwa namba za muhimu zaidi:
I - 1
V - 5
X - 10
L - 50
C - 100
D - 500
M - 1000
Kuunganisha alama za namba[hariri | hariri chanzo]
Kujumlisha alama[hariri | hariri chanzo]
Namba kubwa zaidi huonyeshwa kwa kuandika alama inayotakiwa upande wa kulia lakini kamwe alama ileile mara nne si zaidi ya mara tatu:
I = 1; II = 2; V ni 5 lakini VI ni 6; XX ni 20 lakini XXI ni 21.
Walikuwa na utaratibu wa kutoandika zaidi ya alama tatu ya aina ileile mfululizo. Lakini waliweza kupuuza utaratibu huu pia na kuandika VIIII (9) badala ya IX au XXXX (40) bafala ya XL.
Kupunguza alama[hariri | hariri chanzo]
Namba ndogo zaidi huonyeshwa kwa kuandika alama ndogo upande wa kushoto:
V ni 5 lakini IV ni 4; X ni 10 lakini IX ni tisa
Hapa walifuata utaratibu ufuatao: kuweka I moja au X moja au C moja tu kabla ya alama kuwba zaidi; halafu namba hii yatolewa kwenye namba kubwa:
-
- Mfano: IX=9; LIV=54; XC=90; CD=400; CM=900
I pekee huwekwa kabla ya V au X; X pekee kabla ya L au C; C pekee kabla ya D au M.
-
- Mfano: XCIX (99) lakini siyo IC; CMXCIX (999) lakini siyo IM
Namba mfululizo[hariri | hariri chanzo]
| Alama | Namba | Alama | Namba | Alama | Namba | Alama | Namba |
|---|---|---|---|---|---|---|---|
| I | 1 | XI | 11 | XXX | 30 | CC | 200 |
| II | 2 | XII | 12 | XL | 40 | CCC | 300 |
| III | 3 | XIII | 13 | L | 50 | CD | 400 |
| IV | 4 | XIV | 14 | LX | 60 | D | 500 |
| V | 5 | XV | 15 | LXIX | 69 | DC | 600 |
| VI | 6 | XVI | 16 | LXX | 70 | DCLXVI | 666 |
| VII | 7 | XVII | 17 | LXX | 80 | DCC | 700 |
| VIII | 8 | XVIII | 18 | CX | 90 | DCCC | 800 |
| IX | 9 | XIX | 19 | XCIX | 99 | CM | 900 |
| X | 10 | XX | 20 | C | 100 | M | 1000 |