Nenda kwa yaliyomo

Naledi Pandor

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Naledi Pandor (née Matthews; alizaliwa 7 Desemba 1953) ni mwanasiasa, mwalimu na msomi wa Afrika Kusini ambaye alihudumu kama Waziri wa Mahusiano na Ushirikiano wa Kimataifa kuanzia 2019 hadi 2024. Pia alihudumu kama Mbunge wa African National Congress (ANC) kuanzia 1994 hadi 2024.

Alizaliwa Durban na alisoma elimu ya sekondari nchini Botswana. Baadaye alihitimu kama mwalimu na kufundisha katika shule na vyuo mbalimbali, huku akiendelea kupata shahada tofauti kutoka vyuo vikuu.

Mnamo 1994 aliteuliwa kuwa Mbunge, na mwaka uliofuata (1995) akawa Naibu Mjumbe Mkuu wa ANC. Mnamo 1998 alichaguliwa kuwa Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Kitaifa la Mikoa, na mwaka 1999 akawa mwenyekiti wake.

Katika serikali ya kitaifa, aliteuliwa kuwa Waziri wa Elimu mwaka 2004 chini ya Rais Thabo Mbeki. Aliendelea kuhudumu katika baraza la mawaziri chini ya Kgalema Motlanthe, kisha Rais Jacob Zuma akamteua kuwa Waziri wa Sayansi na Teknolojia mwaka 2009.

Mnamo 2012 alihamishwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, kisha akarudi tena kama Waziri wa Sayansi na Teknolojia mwaka 2014 hadi 2018. Baada ya hapo, chini ya Rais Cyril Ramaphosa, aliteuliwa kuwa Waziri wa Elimu ya Juu na Mafunzo.

Baada ya uchaguzi wa 2019, aliteuliwa kuwa Waziri wa Mahusiano na Ushirikiano wa Kimataifa hadi 2024. Hakuchaguliwa tena katika Bunge katika uchaguzi mkuu wa 2024.

Baadaye alihudumu kama mwenyekiti wa bodi ya wadhamini wa Wakfu wa Nelson Mandela kuanzia Oktoba 2024, na mwaka 2026 aliteuliwa kuwa Chansela wa Chuo Kikuu cha Nelson Mandela, akiapishwa rasmi Aprili 2026.

Maisha ya awali na elimu

[hariri | hariri chanzo]

Naledi Pandor (née Matthews) alizaliwa tarehe 7 Desemba 1953 huko Durban, katika mkoa wa zamani wa Natal, akiwa mtoto wa Regina Thelma (aliyefariki 2002) na Joe Matthews, mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi na mtoto wa msomi Z. K. Matthews (19011968).[1][2] Alipata elimu yake ya msingi na sekondari nchini Botswana, ambapo alihitimu kutoka Shule ya Upili ya Gaborone. Kati ya 1973 na 1977, alipata Cheti cha Elimu Endelevu na Shahada ya Kwanza kutoka University of Swaziland na University of Botswana.[3][4]

Baadaye alisoma ng’ambo na kuhitimu Stashahada ya Elimu na Shahada ya Uzamili kutoka University of London kati ya 1978 na 1979.[5]

  1. "Former deputy minister Joe Matthews dies". Mail & Guardian. 19 Agosti 2010.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. "Minister Naledi Pandor's father, Joe Matthews, dies". South African Government. Iliwekwa mnamo 23 Septemba 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. Petersen, Tammy (16 Aprili 2019). "Minister Pandor walks the walk, graduating with PhD in Education". News24. Iliwekwa mnamo 23 Septemba 2019.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  4. "LOOK: 'She continues to inspire us': Naledi Pandor awarded PhD". IOL. Pretoria, Gauteng. 16 Aprili 2019. Iliwekwa mnamo 23 Septemba 2019.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  5. "Higher education's Naledi Pandor caps string of qualifications with doctorate". TimesLIVE. 16 Aprili 2019. Iliwekwa mnamo 23 Septemba 2019.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Naledi Pandor kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.