Myunga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Kata ya Myunga
Nchi Tanzania
Mkoa Songwe
Wilaya Momba
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 20,814

Myunga ni kata ya Wilaya ya Momba katika Mkoa wa Songwe, Tanzania. Msimbo wa posta ni 53910.

Katika kata hiyo kuna mto mkubwa uitwao Mto Momba.

Kata hii ina jumla ya vijiji saba ambavyo ni Myunga, Lwasho, Mpui, Isunda, Machindo, Mfuto na Namsinde II.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 20,814 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 11,591.[2] walioishi humo.

Shughuli kuu katika kata hii ni kilimo. Mazao yanayolimwa ni kama vile, mahindi, alizeti, maharage, karanga, mpunga n.k.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.nbs.go.tz, uk 231
  2. "Sensa ya 2012, Mbeya - Momba DC". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-03-03. Iliwekwa mnamo 2017-03-15. 
Kata za Wilaya ya Momba - Mkoa wa Songwe - Tanzania

Chilulumo | Chitete | Ikana | Ivuna | Kamsamba | Kapele | Mkomba | Mkulwe | Mpapa | Msangano | Myunga | Ndalambo | Nkangamo | Nzoka


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Songwe bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Myunga kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari .
Usiingize majina ya viongozi au maafisa wa sasa maana wanabadilika haraka mno