Shirikisho la Mataifa ya Sahel
| Shirikisho la Mataifa ya Sahel Confédération des États du Sahel (CES)) | |
|---|---|
| Mji mkubwa | Bamako |
• Rais | Assimi Goïta |
| Wanachama | Burkina Faso Mali Niger |
• Iliundwa | 6 Julai 2024 |
| Eneo | |
| • Jumla | km2 2,781,392 |
| Idadi ya watu | |
| • Kadirio la 2023 | 71,375,590 |
| • Msongamano | 25.7/km2 |
| PLT (PPP) | Kadirio la 2023 |
| • Jumla | $179.37 Bilioni |
| • Kwa kila mtu | $2,513 |
| PLT (Kawaida) | Kadirio la 2023 |
| • Jumla | $62.38 Bilioni |
| • Kwa kila mtu | $874 |
| HDI (2022) | 0.420 (ya 187) chini |
| Sarafu | Faranga ya Afrika ya Magharibi |
| Majira ya saa | UTC+0/+1 GMT |
Shirikisho la Mataifa ya Sahel (kwa Kifaransa: Confédération des États du Sahel, CES, awali: Alliance des États du Sahel, AES) ni shirikisho lililoundwa kati ya Mali, Niger, na Burkina Faso[1][2] baada ya mkataba wa ulinzi wa pamoja uliosainiwa tarehe 16 Septemba 2023, kufuatia mzozo wa kisiasa wa Niger mwaka huo ambayo ilifanya Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) kutishia kuingilia kijeshi kurejesha utawala wa kiraia baada ya mapinduzi nchini Niger. Mataifa yote matatu yaliwahi kuwa wanachama wa ECOWAS lakini baadaye yakajiondoa, huku serikali zao zikiwa chini ya uongozi wa wanajeshi waliochukua madaraka kupitia mapinduzi ya Burkina Faso ya Septemba 2022 na ya Niger ya 2023. Kufuatia misukosuko hii ya kisiasa, mataifa haya yalizidi kushirikiana kijeshi na kisiasa, hatimaye yakatangaza kuunda shirikisho lao rasmi tarehe 6 Julai 2024.
Katika eneo la AES, kuna makundi mbalimbali ya kigaidi na waasi, yakiwemo ISSP, Jama'at Nasr al-Islam wal Muslimin, na makundi mbalimbali ya wanaharakati wa kujitenga yanayopigana Kaskazini mwa Mali kama vile Harakati ya Azawad. Vita dhidi ya makundi hayo vimekuwa vikisaidiwa na wanajeshi wa Ufaransa na Marekani, pamoja na msaada zaidi kutoka kwa vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa. Mnamo mwaka 2024, AES ilikata mahusiano ya kijeshi na mataifa ya Magharibi na kubadilisha majeshi ya Magharibi katika ardhi yao na mamluki wa Urusi, hasa kundi la Wagner.
Muhtasari
[hariri | hariri chanzo]Lengo lililotangazwa na shirikisho hili ni kuunganisha rasilimali ili kujenga miundombinu ya nishati na mawasiliano, kuanzisha soko la pamoja, kutekeleza muungano wa kifedha chini ya sarafu iliyopendekezwa, kuruhusu uhuru wa kusafiri kwa watu, kuwezesha viwanda, na kuwekeza katika kilimo, migodi, na sekta ya nishati, huku lengo la mwisho likiwa ni kuungana kuwa taifa moja huru lenye mamlaka kamili.
Shirikisho hili linapinga ukoloni mamboleo na limethibitisha msimamo wake kupitia hatua kama vile kubadilisha majina ya mitaa ya kikoloni. Pia lina mtazamo wa kupinga Ufaransa na ECOWAS, kwani halikubaliani na sera nyingi za mashirika haya.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "West Africa bloc warns of 'disintegration' as juntas form 'Confederation of Sahel States'". france24.org (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-03-23.
- ↑ Rfi. "Muungano wa Mataifa ya Sahel kukutana mara ya Kwanza mjini niamey" (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-03-23.