Musa Mwarabu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Musa Mwarabu aliishi miaka mingi ya karne ya 4 kama mkaapweke maarufu kati ya Misri na Syria,[1] kabla hajafanywa askofu wa kwanza wa Kiarabu kati ya Waarabu kutokana na sharti la malkia wao, Mavia, kwa ajili ya kusimamisha mapigano yake na Dola la Roma.[2]

Kama askofu Musa hakuwa na makao maalumu, bali alifuata tabia ya uhamaji wa watu wake, akiwaongoa wengi na kudumisha amani kati yao, tena kati yao na dola hilo.[1]

Alifariki mwaka 389 hivi.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Februari[3][4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 Butler and Burns, 2000, p. 68.
  2. Jensen, 1996, pp. 73-75.
  3. Martyrologium Romanum
  4. Bunson et al., 2003, p. 595.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Ball, Warwick (2001), Rome in the East: The Transformation of an Empire, Routledge, ISBN 0-415-11376-8 
  • Bunson, Matthew; Bunson, Margaret; Bunson, Stephen (2003), Our Sunday Visitor's Encyclopedia of Saints, Our Sunday Visitor Publishing, ISBN 1-931709-75-0 
  • Butler, Alban; Burns, Paul (2000), Butler's Lives of the Saints, Continuum International Publishing Group, ISBN 0-86012-251-4 
  • Jensen, Anne (1996), God's Self-confident Daughters: Early Christianity and the Liberation of Women, Westminster John Knox Press, ISBN 0-664-25672-4 
  • Shahîd, Irfan (1995), Byzantium and the Arabs in the Sixth Century, Dumbarton Oaks, ISBN 0-88402-284-6 
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.