Nenda kwa yaliyomo

Mtumiaji:Nezami Ganjavi Mwajemi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nizami Ganjavi

Nizami Ganjavi (Kiajemi: نظامی گنجوی, Kwa Kirumi: Niẓāmī Ganjavī, Kihalisia. 'Niẓāmī wa Ganja') aliishi (c. 1141–1209), Nizami Ganje'i, Nizami, au Nezāmi. Jina lake lilikuwa Jamal ad-Dīn Abū Muḥammad Ilyās ibn-Yūsuf ibn-Zakkī, alikuwa Mwajemi wa karne ya 12, mshairi Muislamu wa dhehebu la Sunni. Nezāmi anachukuliwa kuwa mshairi mashuhuri wa kimahaba katika fasihi ya Kiajemi, ambaye alileta mtindo wa mazungumzo na wa kweli kwa utenzi wa Kiajemi. Turathi zake zinathaminiwa sana na kushirikishwa katika nchi za Afghanistan, Azerbaijan, Iran, eneo la Kurdistan na Tajikistan.


WASIFU Jina lake halisi lilikuwa Ilyas na jina lake la utunzi lilikuwa Nezami (pia limeendelezwa kama Nizami au Neẓāmi). Alizaliwa katika asili ya mjini huko Ganja (eneo la Seljuq, ambalo sasa ni Azerbaijan) na inaaminika kuwa alitumia maisha yake yote huko Caucasus Kusini. Kulingana na De Blois, Ganja lilikuwa jiji ambalo wakati huo lilikuwa na wakazi wengi wa Iran. Mwanahistoria wa Kiarmenia, Kirakos Gandzaketsi (Karne 1200 – 1271) anataja kwamba: "Mji huu ulikuwa na watu wengi wa Iran ikiwemo idadi ndogo ya Wakristo”. Kwa sababu Nezami hakuwa mshairi wa mahakama, haonekani katika kumbukumbu za nasaba. Tazkerehs, ambazo ni mkusanyiko wa kumbukumbu za kifasihi zinazojumuisha kanuni za washairi wakuu pamoja na maelezo ya wasifu na maelezo ya mitindo, humrejelea kwa ufupi sana. Nyingi ya nyenzo hizi katika Tazkereh zinatokana na hekaya, hadithi, na tetesi. Kwahivyo, mambo machache yanajulikana kuhusu maisha ya Nezami, chanzo pekee ikiwa kazi yake mwenyewe, ambayo haitoi taarifa nyingi kuhusu maisha yake binafsi.


Wazazi Nezami aliachwa yatima mapema na alilelewa na mjomba wake, Khwaja Umar ambaye alichukua jukumu la kumlea na kumpa elimu bora. Mama yake, aliyeitwa Ra'isa, alikuwa wa asili ya Kikurdi. Baba yake, ambaye jina lake lilikuwa Yusufu linatajwa mara moja na Nezami katika ushairi wake. Katika mstari huo huo, Nezami anataja jina la babu yake kama Zakki. Katika sehemu ya aya hiyo hiyo, baadhi wamelichukua neno Mu'ayyad kama cheo cha Zakki wakati wengine wamelifasiri kama jina la babu yake mkubwa. Vyanzo vingine vimesema kuwa babake huenda alitoka Qom. Nezami anatajwa kwa namna mbalimbali kama Mwajemi na/au Mwarani.


Familia Nezami alioa mara tatu. Mkewe wa kwanza alikuwa kijakazi wa kabila la Kipchak ambaye alitumwa kwake na Fakhr al-Din Bahramshah, mtawala wa Darband, kama sehemu ya zawadi yake kubwa zaidi. Kwa mujibu wa Iraj Bashiri alikua mke ambaye ni "kipenzi chake zaidi" cha Nezami. Mwanawe wa pekee Mohammad alitoka kwa mke huyu. Mkewe alikufa baada ya shairi la ‘Khosrow na Shirin’ kukamilika. Muhammad alikuwa na umri wa miaka saba wakati huo. Nezami anamtaja mwanawe tena katika shairi lake la ‘Layli na Majnun’ akiongeza kuwa sasa mwana huyu ana umri wa miaka 14 na ‘kipenzi chake’. Katika tenzi lake la "Haft Peykar" (Warembo Saba), pia anamtaja na kumshauri mwanawe kuhusu kuchukua jukumu zaidi kwani baba alikuwa akidhoofika zaidi.

Baadhi ya waandishi wa kisasa mwishoni mwa karne ya 20 wamedai kuwa mke huyu aliitwa Afaq. Vahid Dastgerdi anaonekana kuwa mwandishi wa kwanza kupendekeza jina kuwa ni la mke wa kwanza wa Nezami, lakini Said Nafisi (wakati huo huo) na chanzo cha hivi karibuni kimepinga tafsiri hii ya aya inayolingana katika kazi ya Nezami na kudhani kuwa Afaq lilikuwa jina halisi la mke wake na wamechukua Afaq katika aya hiyo kumaanisha tu ‘upeo wa macho’ badala ya jina sahihi. Cha ajabu, wake wengine wawili wa Nezami, pia, walikufa kabla ya wakati - kifo cha kila mmoja kiliendana na kukamilika kwa tenzi, na kumfanya mshairi kusema, "Mungu, kwa nini kwa kila mathnawi lazima nimtoe mke dhabihu!"


Elimu Nezami hakuwa mwanafalsafa kiwango cha Avicenna au mfafanuzi wa Usufi wa kinadharia kwa maana ya Ibn ‘Arabi’. Hata hivyo, anachukuliwa kuwa mwanafalsafa na mwagnostiki ambaye alibobea katika nyanja mbalimbali za fikira za Kiislamu ambazo alizikusanya kwa njia inayoleta akilini mila za ‘wenye hekima’ wa baadaye kama vile Qutb al-Din Shirazi. Mara nyingi hurejelewa na Mwadhamu Hakim (‘Mwenye hekima’), kuwa Nezami ni mshairi msomi na aliyebobea kwa mitindo ya sauti na msisimko. Hakuna shaka kuhusu kujifunza kwa Nezami kwa ustadi. Washairi walitarajiwa kufahamu vyema masomo mengi; lakini Nezami inaonekana kuwa msomi wa kipekee. Mashairi yake yanaonyesha kwamba sio tu kwamba alifahamu fasihi za Kiarabu na Kiajemi kikamilifu na mila za simulizi na maandishi maarufu na za kienyeji, bali pia alifahamu fani mbalimbali kama vile hisabati, unajimu, alkemia, dawa, botania, ufafanuzi wa Kurani, nadharia na sheria ya Kiislamu, hekaya na hekaya za Kiirani, historia, maadili, falsafa na fikra za kisomi, muziki, na sanaa. Tabia yake dhabiti, uhamasishaji wa kijamii, na ujuzi wa rekodi za simulizi na maandishi, pamoja na torathi thabiti za kitamaduni za Kiajemi unaunganisha Iran ya kabla ya Uislamu na Iran ya Kiislamu katika kuunda kiwango kipya cha mafanikio ya kifasihi. Akiwa ni zao la utamaduni wa Kiirani wa wakati huo, sio tu aliunda daraja kati ya Iran ya kabla ya Uislamu na Iran ambayo ni ya Kiislamu, bali pia kati ya Iran na ulimwengu wote wa kale.

Athari na ukumbi wa fasihi Ugunduzi na uchapishaji wa hivi majuzi wa mkusanyiko wa kazi za fasihi simulizi na andishi wenye jina la ‘Nozhat al-Majales’ (Furaha ya Mikusanyiko) ina lugha ya kiajemi kutoka kwa Nizami na washairi wengine 115 kutoka kaskazini-magharibi mwa Iran (Arrān, Šarvān, Azerbaijan; ikiwa ni pamoja na washairi 24 kutoka Ganja pekee) katika enzi hiyo hiyo. Tofauti na sehemu nyingine za Uajemi, ambako washairi wengi walikuwa wa tabaka za juu za jamii kama vile wasomi, warasimu, na makatibu, idadi kubwa ya washairi katika maeneo ya kaskazini-magharibi iliongezeka kutoka miongoni mwa watu wa kawaida wenye malezi ya tabaka la wajakazi, na walitumia mara kwa mara semi za mazungumzo katika ushairi wao. Ipasavyo, kitabu hiki kinaonyesha hali ya kijamii wakati huo, ikionyesha kuenea kamili kwa lugha ya Kiajemi na utamaduni katika eneo hilo, ambayo inathibitishwa na matumizi ya kawaida ya nahau simulizi katika mashairi na taaluma za washairi wengi. Ushawishi wa lugha ya Kipahlavi ya kaskazini-magharibi, kwa mfano, ambayo ilikuwa ni lahaja inayozungumzwa eneo hilo, inaonekana wazi katika mashairi yaliyo katika antholojia hii. Hata hivyo, wakati huo huo, eneo la Caucasus lilikuwa likiburudisha mchanganyiko wa kipekee wa mchanganyiko wa tamaduni za kikabila mengi. Mama yake Khaqani alikuwa Mkristo wa Nestoria, mama yake Mojir Baylqani alikuwa Mwarmenia, na mamake Nezami alikuwa Mkurdi. Kazi zao zinaonyesha tofauti za kitamaduni na lugha za eneo hilo.


Utamaduni wa Kiajemi Athari za kazi za Neẓāmi juu ya maendeleo ya baadae ya fasihi ya Kiajemi umekuwa mkubwa na Khamseh akawa mtindo ambao ulioigwa katika ushairi wa baadaye wa Kiajemi (na pia katika fasihi nyingine za Kiislamu). Hiba ya Nezami umeonekana sana katika ulimwengu wa Kiislamu na ushairi wake umeathiri maendeleo ya mashairi ya Kiajemi, Kiarabu, Kituruki, Kikurdi na Kiurdu miongoni mwa lugha nyingine nyingi. Katika historia ya uchoraji wa picha ndogo za Kiajemi, hadithi katika mashairi ya Nezami pamoja na yale ya Shahnameh ya Ferdowsi zimekuwa kazi za fasihi zinazoonyeshwa mara kwa mara. Kulingana na Kamusi elezi ya Britannica, Nezami "anavutia katika nchi zinazozungumza Kiajemi kwa uasilia wake na uwazi wa mtindo, ingawa upendo wake wa lugha kwa ajili yake na kujifunza kifalsafa na kisayansi hufanya kazi yake kuwa ngumu kwa msomaji wa kawaida." Nezami alitunga beti zake katika lugha ya Kiajemi na ensaiklopidia za Magharibi kama vile Ensaiklopidia ya Uislamu, Ensaiklopidia Iranica, Ensaiklopidia Britannica na wataalamu wa mambo ya nchi nyingi za mashariki wanamchukulia Nezami kama mshairi muhimu wa Kiajemi na mweledi kwa uimbaji wa shairi za kimahaba katika fasihi ya Kiajemi.