Mtolondo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtolondo
Dume la Mtolondo domo-jekundu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Passeroidea (Ndege kama shomoro)
Familia: Estrildidae (Ndege walio na mnasaba na mishigi)
Jenasi: Lagonosticta
Cabanis, 1851
Ngazi za chini

Spishi 11:

Mitolondo au bwerenda ni ndege wadogo wa jenasi Lagonosticta katika familia Estrildidae ambao wanatokea Afrika tu. Wanafana na mishigi lakini madume wana rangi za nyekundu, kahawa na kijivu, pengine pamoja na madoa meupe madogo. Majike wana rangi za kahawa na kijivu kwa kawaida lakini mara nyingi wana sehemu nyekundu pia na madoa meupe kidarini. Hula mbegu hasa na wadudu pia, hususa makinda. Tago lao ni tufe la manyasi na majani lenye mwingilio kwa kando. Jike huyataga mayai 3-6. Spishi nyingi ni wateswa wa vinili ambao huyataga mayai yao katika matago ya mitolondo.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]