Kizito
Mandhari
(Elekezwa kutoka Mtakatifu Kizito)


Kizito (1872 - Namugongo, Uganda, 3 Juni 1886) ni mmojawapo wa Wafiadini wa Uganda, mdogo kuliko wote. Alichomwa moto kwa ajili ya imani yake kwa Yesu Kristo akiwa na umri wa miaka 14 tu. Kidogo tu kabla hajauawa alibatizwa na katekista Karolo Lwanga [1].
Pamoja na wenzake alitangazwa na Papa Benedikto XV kuwa wenye heri tarehe 6 Juni 1920, halafu na Papa Paulo VI kuwa mtakatifu tarehe 18 Oktoba 1964 huko Roma.
Sikukuu yake ni tarehe 3 Juni kila mwaka[2].
Ni msimamizi wa watoto na wa shule za msingi.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- J. FRANSE, W.F., Mashahidi 22 wa Uganda – tafsiri ya C. Kuhenga n.k. – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1981
- John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 190-194
- Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 160-162
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Saint Kizito Ilihifadhiwa 16 Juni 2008 kwenye Wayback Machine. at Patron Saints Index
- Kizito's profile from Dictionary of African Christian Biography Ilihifadhiwa 13 Desemba 2016 kwenye Wayback Machine.
- Kizito's profile from UgandaMartyrsShrine.org Ilihifadhiwa 17 Machi 2014 kwenye Wayback Machine.
- The Uganda Martyrs from the August 2008 issue of The Word Among Us magazine Ilihifadhiwa 23 Agosti 2018 kwenye Wayback Machine.
| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |