Motown Records

Motown ni lebo ya muziki ya Marekani inayomilikiwa na Universal Music Group. Ilianzishwa na Berry Gordy Jr. kama Tamla Records mnamo Januari 12, 1959, na baadaye kusajiliwa kama Motown Record Corporation mnamo Aprili 14, 1960.[1] Jina "Motown" ni muunganiko wa maneno motor na town, ambalo limekuwa jina la utani la mji wa Detroit, kitovu cha tasnia ya magari nchini Marekani, ambako lebo hiyo ilianzia.[2]
Motown ilicheza rasilimali muhimu katika kuchanganya mbari za wanamuziki katika muziki wa pop, ikiwa ni lebo inayomilikiwa na Waamerika mweusi iliyopata mafanikio makubwa kwa watazamaji weupe. Katika miaka ya 1960, Motown ilivuma kwa mtindo wa Motown sound, aina ya muziki wa soul uliokuwa na ushawishi wa miondoko ya pop. Kati ya mwaka 1960 na 1969, nyimbo 79 za Motown zilifikia kumi bora kwenye chati za Billboard Hot 100.
Baada ya machafuko ya Detroit ya mwaka 1967 na kuondoka kwa timu muhimu ya waandishi Holland–Dozier–Holland, Gordy alihamishia makao makuu ya Motown kwenda Los Angeles, California, na kuanza kujishughulisha na utengenezaji wa filamu na televisheni. Kampuni hiyo ilibaki huru hadi mwaka 1988 iliponunuliwa na MCA Records, na baadaye kupitia mikononi mwa PolyGram kabla ya kuchukuliwa na Universal Music Group mwaka 1999.[1]
Mnamo mwaka 2014, Motown ilihamia ndani ya Capitol Music Group huko Los Angeles, ikifanya kazi kutokea jengo la Capitol Tower.[3] Mwaka 2021, lebo hiyo ilitengana na Capitol na kuwa lebo inayojitegemea tena chini ya Universal. Hadi kufikia mwaka 2023, Motown inasimamia wasanii maarufu wa hip hop na R&B kama City Girls, Migos, Lil Baby, Lil Yachty, na YoungBoy Never Broke Again.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- 1 2 Cruz, Gilbert (12 Januari 2009). "A Brief History of Motown". Time. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-02-05. Iliwekwa mnamo 2026-05-02.
{{cite magazine}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ Palmer, Brian (2012-02-29). "How Did Detroit Become Motor City?". Slate.com.
- ↑ "A revitalized Capitol Records forges a new path forward". Los Angeles Times. 2015-02-03.