Mesite

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Monias)
Mesite
Mesite domo-mundu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Mesitornithiformes (Ndege kama mesite)
Familia: Mesitornithidae (Mesite)
Ngazi za chini

Jenasi 2, spishi 3:

Mesite (kutoka Kifaransa: mésite) ni ndege wa familia Mesitornithidae. Undugu wa ndege hawa si wa uhakika. Kwa kawaida huainishwa katika Gruiformes, lakini utafiti wa hivi karibuni umeonyesha kama wana mnasaba zaidi na Columbiformes. Kwa sasa waainishwa katika oda yao yenyewe Mesitornithiformes. Mesite wanafanana na viluwiri wenye miguu na mkia miferu. Rangi yao ni kahawia au kjivu mgongoni na nyeupe au kahawia isioiva chini. Wanatokea Madagaska na hula wadudu, mijusi na vyura wadogo, mbegu na beri. Hulijenga tago lao kwa vijiti katika kichaka na jike huyataga mayai 2-3.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu "Mesite" inatumia neno (au maneno) ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio la kutafsiri neno (au maneno) la asili mésite kutoka lugha ya Kifaransa. Neno (au maneno) la jaribio ni mesite.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.