Mohammad Khatami
Mohammad Khatami (alizaliwa 14 Oktoba 1943) alikuwa mwanasiasa wa Iran na kiongozi wa kidini wa dhehebu la Shia alihudumu kama rais wa tano wa Iran kuanzia tarehe 3 Agosti 1997 hadi 3 Agosti 2005. Pia alihudumu kama Waziri wa Utamaduni wa Iran kuanzia mwaka 1982 hadi 1992. Baadaye, alikuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya rais aliyemfuata, Mahmoud Ahmadinejad.
Akiwa hajulikani sana kimataifa kabla ya kuwa rais, Khatami alivutia umakini mkubwa wakati wa uchaguzi wake wa kwanza wa urais ambapo alipata karibu 70% ya kura zote.[1] Khatami aligombea akilenga kuleta uhuru wa kijamii na mageuzi. Wakati wa kampeni zake za uchaguzi, Khatami alipendekeza wazo la Mazungumzo Kati ya Miundo ya Jamii (Dialogue Among Civilizations) kama jibu kwa nadharia ya mwaka 1992 ya Samuel P. Huntington inayohusu Mgongano wa Miundo ya Jamii (Clash of Civilizations).[2] Umoja wa Mataifa baadaye ulitangaza mwaka 2001 kuwa Mwaka wa Mazungumzo Kati ya Miundo ya Jamii, kufuatia mapendekezo ya Khatami.[3][4][5] Katika vipindi vyake viwili kama rais, Khatami alitetea uhuru wa kujieleza, uvumilivu na asasi za kiraia, uhusiano mzuri wa kidiplomasia na mataifa mengine ikiwemo yale ya Asia na Umoja wa Ulaya, pamoja na sera ya kiuchumi iliyounga mkono soko huria na uwekezaji wa kigeni.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Profile: Mohammad Khatami". BBC News. 6 Juni 2001. Iliwekwa mnamo 20 Mei 2013.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Khatami Speaks of Dialogue among Civilizations". diplomacy (kwa Kiingereza). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2022-10-24. Iliwekwa mnamo 11 Oktoba 2021.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Dialogue among Civilizations". UNESCO. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 5 Februari 2007.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Round Table: Dialogue among Civilizations United Nations, New York, 5 September 2000 Provisional verbatim transcription". UNESCO. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 10 Machi 2007.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ Petito, Fabio (2004). "Khatami' Dialogue among Civilizations as International Political Theory" (PDF). International Journal of Humanities. 11 (3): 11–29.
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mohammad Khatami kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |