Mnyama
Wanyama | ||||
---|---|---|---|---|
Wanyama mbalimbali; kutoka juu-kushoto mpaka chini-kulia: kiti cha pweza, sifongo-bahari, ngisi kibete, konyeza, nondo-chui, mwata, kombe-taa, chui milia, mfoko-bahari, kidudu-dubu, mnyama-kigoga, mkunga-chui, kaa, daa kichwa-miiba, kunguru buluu, buibui mrukaji, mnyoo-bapa bahari, daa-upepeo.
| ||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||
| ||||
Ngazi za chini | ||||
|
Wanyama ni viumbehai wasio mmea. Jina la kisayansi ni animalia (kutoka Kilatini).
Hawapati chakula chao kupitia usanisinuru (nishati ya jua) lakini kutoka kwa viumbehai vingine ama wanyama wengine au mimea.
Wanyama wanahitaji oksijeni kwa kupumua.
Wanyama walio wengi hutembea yaani hubadilisha mahali wanapokaa, kwa hiyo wanahitaji milango ya maarifa.
Sayansi inayochunguza wanyama huitwa zoolojia, ambayo ni tawi la biolojia.
Wala mimea huitwa herbivori na wala nyama huitwa karnivori. Kuna pia wanyama wanaoitwa omnivori yaani wanakula kila kitu ama mimea au wanyama wengine.
Aina za wanyama ni nyingi sana. Mara nyingi aina zao zinatofautishwa kama ni wanyama wenye seli nyingi (metazoa) au seli moja (protozoa) tu.
Kuna wanyama wanaoishi peke yao, katika vikundi na jamii. Mfano wa wanyama wanaoishi peke yao ni kifaru au nyoka. Wanajumuika kwa tendo la kuzaa pekee. Mfano wa wanyama wa jumuiya ni simba wanaokaa na kuwinda pamoja. Ushirikiano unasaidia kupata chakula bora. Mfano wa wanyama katika jamii ni nyuki na wadudu wengine.
Upande wa mwili hata binadamu ni mnyama na kimaumbile anahesabiwa kati ya mamalia.
Viungo vya nje
Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mnyama kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |