Mnara wa taa wa Barra

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mnara wa taa wa Barra ni mnara wa taa wa pili kujengwa huko Barra kwenye mji wa Salvador, jimbo la Bahia, nchini Brazil. Mnara wa kwanza kwenye nafasi hii ulijengwa kwa udongo ulioshindiliwa, na ulikuwa mnara wa taa wa pili kujengwa Amerika, baada ya mnara wa zamani wa Jumba la Fribourg huko Recife. Mnara wa sasa ulijengwa mnamo mwaka 1839 na kutolewa na Dom Pedro II wa Brazil. Umejengwa kwa uashi na kupakwa rangi kwa bendi nyeusi na nyeupe. Mnara wa taa una mrefu wa mita 22 na taa yake iya mwaka 1890 ina lenzi ya Fresnel. Mnara huu lijengwa ndani ya ngome iliyolinda mdomo wa bandari. Ngome pamoja na mnara wa taa ziliorodheshwa kama miundo ya kihistoria na Taasisi ya Urithi wa Kihistoria na Usanii mnamo mwaka1938

Mnara wa taa wa kwanza[hariri | hariri chanzo]

Mnara wa taa wa kwanza wa huko Barra ulijengwa kwa sababu ya upanuzi wa biashara za utumwa huko Bahia katika karne ya 17. Bandari ya huko Salvador ilikuwa ni hatua kuu ya biashara ya watumwa wa Atlantiki huko Brazil. Mkoa huo, kwa upande wake, ulitumika kusafirisha sukari, pamba, tumbaku, na mbao kwa soko la watumiaji wa Uropa. Galeão Santíssimo Sacramento alipata ajali mbaya ya meli mnamo Mei 5, mwaka 1668 kwenye ukingo wa mchanga kwenye mdomo wa Mto Vermelho kwa sababu ya ukosefu wa mnara wa taa katika eneo hilo. Ngome ya Santo Antônio da Barra, ambayo ilijengwa upya mnamo mwaka 1696 chini ya serikali ya João de Lencastre (1694-1702), ulijenga katika pembe nne katika ngome iliyokuwa na taa ya shaba iliyokuwa na glasi. Sura ya mraba ya mnara wa taa, tofauti na muundo wa leo, inaonekana katika "Cartas Soteropolitanas" mwishoni mwa karne ya 18 na Luís dos Santos Vilhena. Ilikuwa inaendeshwa na mafuta ya nyangumi, na ikaitwa Vigia da Barra au Farol da Barra.

Kitabu cha Kiingereza cha William Dampier, cha mwaka 1699, kilirekodi: "Mlango wa Todos OS Santos Bay unatetewa na ngome ya Santo Antônio, ambapo taa zake zimewekwa na kusimamishwa kwa ajili ya kuongoza meli, ambazo zinaonekana usiku. "

Mnara wa taa wa pili[hariri | hariri chanzo]

mnara wa taa wa Barra,1922

Baada ya utawala wa Wareno kutoka kwa Amri ya udhibiti ya Brazil ya Julai 6, mwaka 1832 ikiagiza kuwekwa kwa taa ya kisasa zaidi huko Barra. Serikali iliamuru mnara wa taa uliotengenezwa nchini Uingereza kuchukua nafasi ya ile ya zamani. Iliwekwa wakfu na Dom Pedro II mnamo Desemba 2, mwaka 1839. iliyowashwa na mafuta ya taa, na ilionekana kwa maili kumi na nane ya baharini katika hali ya hewa safi. Mfumo wa zamani wa mnara wa taa twa "Barbier" ilibadilishwa na taa ya umeme mnamo mwaka 1937.

Hali iliyohifadhiwa[hariri | hariri chanzo]

Santo Antônio da Barra Fort na Barra ni mnara wa taa unalindwa kama muundo wa kihistoria na Taasisi ya Kitaifa ya Urithi wa Kihistoria na Usanii. Ngome hiyo iliorodheshwa kama muundo wa kihistoria mnamo mwaka 1938.

Ufikiaji[hariri | hariri chanzo]

Mnara wa Taa wa Barra, tofauti na mingine huko Brazil, uko wazi kwa umma na inaweza kutembelewa.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]