Mlangobahari wa Bering

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mlango wa Bering)
Mlangobahari wa Bering unavyoonekana kutoka angani
Ramani ya mlangobahari wa Bering

Mlangobahari wa Bering (kwa Kirusi: Берингов пролив; kwa Kiingereza: Bering Strait) ni mlango wa bahari na mahali pa kukaribiana kati ya Alaska upande wa Amerika ya Kaskazini na Siberia upande wa Asia.

Mlangobahari wa Bering una upana wa takriban kilomita 92 na kina cha mita 30 hadi 50 pekee. Unaunganisha bahari ya Aktiki na Pasifiki.

Jina limetokana na Vitus Bering aliyekuwa Mdenmark katika utumishi wa Urusi aliyevuka mlangobahari huo mwaka 1728.

Kando ya mlangobahari wa Bering pande zote mbili maeneo yana watu wachache kwa sababu ya mazingira ya baridi.

Kufuatana na nadharia za wataalamu wa historia hapa palikuwa mahali pa kuvuka kwa watu wa kwanza kutoka Asia kwenda Amerika. Inafikiriwa ya kwamba wakati wa Enzi ya Barafu miaka 10,000 iliyopita kiasi kikubwa cha maji duniani kilipatikana kwa umbo la barafu na hivyo kiasi cha maji kiowevu kilikuwa kidogo kuliko leo. Kwa sababu hiyo usawa wa bahari ulikuwa takriban mita 121 chini ya uwiano wa leo[1] na mlangobahari wa Bering ulikuwa mkavu ukapitika kwa miguu. Hivyo watu waliingia kwa mara ya kwanza barani Amerika.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. [http://earth.rice.edu/mtpe/cryo/cryosphere/topics/ice_age/ice_sea.html As ice sheets build up sea level drops, exposing continental shelves] Archived 2 Mei 2017 at the Wayback Machine., Tovuti ya rice.edu, ilitazamiwa Februari 2017
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.