Mkizi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkizi
Mkizi mkia-buluu (Crenimugil buchanani)
Mkizi mkia-buluu (Crenimugil buchanani)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Actinopterygii (Samaki walio na mapezi yenye tindi)
Oda: Mugiliformes (Samaki kama mkizi)
Familia: Mugilidae (Samaki walio na mnasaba na mkizi)
Cuvier, 1829
Ngazi za chini

Jenasi 27 na spishi 70, 32 katika Afrika:

Mkizi au binini ni samaki wa baharini na pengine wa maji baridi za familia Mugilidae katika oda Mugiliformes. Wanatokea katika kanda za wastani hadi tropiki. Wana magamba mapana na rangi ya kijivu na hudhurungi mgongoni.

Pengine hanithi huitwa mkizi pia, lakini ni aina tofauti.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Mkizi wanajulikana kwa kuwepo kwa mapezimgongo mawili tofauti, kinywa kidogo cha pembetatu na kutokuwepo kwa mrabafahamu. Hujilisha kwa takataka na spishi nyingi zina tumbo lenye misuli lisilo na kawaida na koromeo tata ili kusaidia umeng'enyaji wa chakula.

Mwenendo[hariri | hariri chanzo]

Mwenendo wa kawaida unaoonekana katika mkizi ni mwelekeo wa kuruka nje ya maji. Kuna aina bainifu mbili za miruko: lengo nyofu na safi kutoka majini ili kuepuka mbuai na mruko polepole na chini zaidi huku akijigeua kwa ubavu wake ambao husababisha mtawanyiko mkubwa zaidi unaoonekana vizuri zaidi. Sababu za mruko huu kwa chini zinakabiliwa, lakini nadharia huwekwa kwamba sababu ni kupata hewa yenye kiwango cha juu cha oksijeni ili kubadilishana gesi katika ogani ndogo juu ya koromeo.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Rashid Anam & Edoardo Mostarda (2012) Field identification guide for the living marine resources of Kenya. FAO, Rome.
  • Gabriella Bianchi (1985) Field guide to the commercial marine brackish-water species of Tanzania. FAO, Rome.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]