Mikaeli wa Sinnada

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mikaeli wa Sinnada (alifariki Şuhut, Frigia, Uturuki wa leo, 23 Mei 826) alikuwa askofu mkuu wa mji huo kuanzia mwaka 784/787 hadi 815.

Alishiriki Mtaguso wa pili wa Nisea (787).

Alikuwa mpatanishi kati ya Wakristo wa Mashariki na wale wa Magharibi.

Alipelekwa uhamishoni na kaisari Leo V kwa sababu ya kutetea matumizi ya picha takatifu[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[2][3].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 23 Mei[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.