Mgongo wa bahari wa Chile

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mgongo wa bahari wa Chile (kwa Kiingereza: Chile Ridge) ni mgongo wa baharini yaani safu ya milima kwenye sakafu ya bahari. Unafuata mpaka baina ya mabamba mawili ya gandunia: bamba la Nazca na bamba la Antaktiki.

Mgongo wa bahari wa Chile unazama chini ya bara la Amerika Kusini kwenye mfereji wa Peru-Chile unaoitwa pia mfereji wa Atamaca. [1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Russo, R.M.; Vandecar, John C.; Comte, Diana; Mocanu, Victor I.; Gallego, Alejandro; Murdie, Ruth E. (2010). "Subduction of the Chile Ridge: Upper mantle structure and flow". GSA Today (Geological Society of America) 20 (9): 4. doi:10.1130/GSATG61A.1.