Nenda kwa yaliyomo

Mervin E. Muller

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mervin Edgar Muller (1 Juni 19283 Desemba 2018) alikuwa mwanasayansi wa kompyuta na mwanahisabati kutoka Marekani. Ubadilishaji wa Box–Muller (Box–Muller transform) umepewa jina lake kwa heshima yake.[1]

Muller alizaliwa mjini Hollywood, , Los Angeles, tarehe 1 Juni 1928, akiwa mmoja wa wana wanne wa wazazi wake Emanuel na Bertha Muller. Wazazi wake wote wawili walikuwa wahamiaji kutoka Hungaria. Alisoma hisabati katika Chuo Kikuu cha California, Los Angeles (UCLA), ambako alipata shahada ya uzamivu (Ph.D.) mwaka 1954 chini ya usimamizi wa George William Brown.[2]

Muller alifanya kazi katika IBM huko New York, na baadaye akafanya kazi kwa miaka kumi na mitano katika Benki ya Dunia (World Bank) mjini Washington, D.C.

Alifundisha katika UCLA, Chuo Kikuu cha Cornell, Chuo Kikuu cha Princeton, Chuo Kikuu cha George Mason, na Chuo Kikuu cha Wisconsin–Madison kabla ya kujiunga na kitivo cha Chuo Kikuu cha Jimbo la Ohio (Ohio State University), ambako alistaafu akiwa na cheo cha Profesa wa Uhandisi wa Robert Critchfield.

Alikuwa na wana watatu pamoja na mke wake Barbara McAdam Muller. Alifariki dunia mjini Columbus, Ohio, tarehe 3 Desemba 2018, akiwa na umri wa miaka 90.[3]

  1. "Mervin Muller - The Mathematics Genealogy Project". www.mathgenealogy.org. Iliwekwa mnamo 12 Februari 2022.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. "Mervin Muller". Columbus Dispatch. 5 Desemba 2018. Iliwekwa mnamo 15 Desemba 2018.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. "Mervin Muller". Columbus Dispatch. 5 Desemba 2018. Iliwekwa mnamo 15 Desemba 2018.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mervin E. Muller kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.