Merlene Ottey
Mandhari
| Merlene Ottey | |
|---|---|
| | |
| Jina la kuzaliwa | Jamaika |
| Alizaliwa | 10/5/1960 |
| Nchi | Jamaika |
Merlene Joyce Ottey (alizaliwa 10 Mei 1960) ni mkimbiaji wa mbio fupi wa zamani wa Jamaica na Slovenia. Alianza kazi yake ya kitaaluma akiwakilisha Jamaica mwaka 1978 na kuendelea kufanya hivyo kwa miaka 24 kabla ya kuwakilisha Slovenia kutoka 2002 hadi 2012. Yupo katika nafasi ya sita kwenye orodha ya muda wote katika mbio za mita 60 (ndani ya jengo), nafasi ya kumi na moja katika mita 100, na nafasi ya saba katika mita 200.[1] Ana rekodi ya dunia ya ndani ya jengo (indoor) kwa mita 200 kwa muda wa sekunde 21.87, iliyowekwa mwaka 1993. Ottey amechaguliwa kuwa Mwanamichezo wa Kike Bora wa Jamaica mara 13 kati ya mwaka 1979 na 1995.[2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Merlene Ottey races in Barcelona at 50 years of age Archived 26 Julai 2010 at the Wayback Machine. Barcelona 2010 official site. Retrieved on 29 July 2010.
- ↑ Agostinho Pinnock (23 Agosti 2005). "Merlene Ottey – no longer going for gold?". Jamaica Observer, newspaper. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 17 Oktoba 2007. Iliwekwa mnamo 4 Agosti 2009.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Merlene Ottey kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |