Mazahr Makatemele
Makala hii inahitaji vyanzo zaidi ili kuwezesha kuonyesha uthibitisho. |
Mazahr Makatemele (takriban 1846–1903) alikuwa mfanyakazi wa nyumbani mwenye asili ya Afrika aliyeishi Uswidi. Alikuwa mtu maarufu katika historia ya mji wa Kalmar na anajulikana kama mmoja wa wanawake wa kwanza wenye asili ya Kiafrika nchini Uswidi ambao maisha yao yameandikwa na kuhifadhiwa katika kumbukumbu rasmi.[1]
Alizaliwa katika koloni la Natal[1], na inaripotiwa kuwa alitoka katika kabila la Watswana au Wasotho. Alitekwa na kuwekwa utumwani na Makaburu mnamo mwaka 1857 au 1858. Hatimaye alikuwa mfanyakazi wa nyumbani wa mfanyabiashara wa Kiswidi aitwaye Alarik Forssman, aliyekuwa akitembelea Afrika Kusini na familia yake.Mazahr aliajiriwa kama mfanyakazi huru na mlezi wa watoto katika familia ya Forssman. Mnamo Mwaka 1862, alisafiri pamoja nao hadi Kalmar, Sweden. Alipofika, alihudumiwa na Swedish Mission Society akabatizwa kuwa Mkristo. Ubatizo wake ulipewa umaarufu mkubwa na ulileta sifa nzuri kwake. Kuanzia mwaka 1864, Mazahr Makatemele aliajiriwa kama mfanyakazi wa ndani na Cecilia Fryxell aliyekuwa na shule ya wasichana.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- 1 2 3 "skbl.se - Mazahr Makatemele". skbl.se (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-07-13.