Masimo wa Torino

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Maximus of Turin)
Mt. Masimo katika mavazi ya ibada ya Kiaskofu.

Masimo wa Torino (labda 380 hivi – 420 hivi) alikuwa askofu wa Kanisa Katoliki na mwanateolojia kutoka Italia Kaskazini.

Mwanafunzi wa watakatifu Eusebi wa Vercelli na Ambrosi wa Milano, alipata kuwa askofu wa Torino, Italia, kwa miaka 30 hivi, tena ndiye wa kwanza kujulikana katika ya maaskofu wake.

Kwa maneno yake ya kibaba alivuta umati wa Wapagani kwenye imani ya Kikristo akawaongoza kwa mafundisho ya Kimungu kwenye tuzo ya wokovu[1].

Alitunga hotuba mia kadhaa [2] na vitabu sita.

Ingawa maisha yake hayajulikani sana, huyo babu wa Kanisa anaheshimiwa tangu zamani kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 25 Juni[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/33400
  2. Corpus Christianorum Series Latina n° XXIII, Turnhout, 1962.
  3. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.